Nuh Mziwanda akiwa na mchumba wake, Shilole
..Maneno ya ‘Sadd na Sadness’, ‘Women na Woman’ yamtatiza
Na Andrew Chale wa Modewji blog
Huenda
hii ikawa ni tabia endelevu kwa baadhi ya mastaa wa Bongo hasa wasanii
wa filamu, muziki na watu maalufu kwa kung’ang’ania kuutukuza
‘Umagharibi’, hasa kwa kupenda kutumia lugha ya Kiingereza ambacho mara
zote kimekuwa kikiwatoa jacho..
Hivi
sasa Nuh Mziwanda ambaye mwenye mahusiano ya uchumba na mwimbaji
Shilole ameibua mijadara huku wengi wakimtupia madongo baada ya kupost
ujumbe aliouandika kwa kiingereza cha mtaani ambacho vijana wa mjini
wanasema cha ‘Kuombea mma au cha kuungauunga’ kupitia mtandao wake wa
kijamii wa Instagram. (TAZAMA Sreen shot hapa chini)..
![11149808_1085556938137392_5917159520963772825_o](http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/11149808_1085556938137392_5917159520963772825_o.jpg)
Posti
aliyoitupia kwenye mtandao wake wa Instagram na kuzua mjadara kwenye
mitandao mingine ya Kijamii ikiwemo ya Facebook,Whatsapp na Twitter na
dewjiblog.com
Hata
hivyo baada ya ujumbe huo kuutupia leo Aprili 11, majira mchana
kupitia akaunti yake ya Instagram, yenye fans wake lukuki, ujumbe huo
ulitembelewa na watu wengi huku zaidi ya 2,000 waki-LIKE, Ambapo pia,
fans wake hao waliweza kuongelea ujumbe huo huku wengi wakimpiga madogo
kwa lugha hiyo aliyoitumia na baadala yake walimtaka kuwa ni bora
angetupia lugha yake ya Kiswahili.
Hata
hivyo ni nadra sana kwa mastaa wa Bongo ama watu maalufu kujibu
komenti za fans wao, lakini kwa hili la Mziwanda lilimshinda aliamua
kuwajibu wote waliompiga madongo kwa kiingereza chake hicho huku
akikitetea. (TAZAMA screen shot hapa chini).
![11137120_10206288399997034_3148340188159438295_n](http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/11137120_10206288399997034_3148340188159438295_n.jpg)
Posti yake
ya kujitetea ambayo nayo mpaka muda huu tunakuwekea hapa tayari imepata
LIKE zaidi ya 1800 na komenti zaidi ya 250 huku wengi wakimsahihisha na
wengine wakimtaka aende akasome english course.
Licha
ya kuwajibu huko ni sawa kama amezima moto kwa kutumia petrol kwani
walimshambulia vikali huku wengi wakimtaka aende darasani akasome
kiingereza.
Tuendeleee
kushirikiana nanyi marafiki wetu katika kuboresha mtandao wetu huu bora
wa habari moto moto kila siku, kila saa muda wote KUWA NASI, PERUZI
NASI. Tutumie habari, Picha na jambo lolote lile kupitia namba za simu
zilizopo hapo juu kulia ama kupitia namba hizi 0719076376 au 0754940992
!!! Kama una Gossip !!!Exclusive tuma Whatsapp 0767076376
Post a Comment