FAMILIA YAKATWA MAPANGA

Tukio hilo lilitokea Aprili 18, mwaka huu, maeneo ya Mkuranga mkoani Pwani ambapo awali familia hiyo ilipata taarifa kuwa kuna watu wanaonekana kwenye shamba lao wakikata miti na kujipimia maeneo, hali iliyowalazimu kufunga safari ili kujua watu hao walikuwa na lengo gani.
Akizungumza na waandishi wetu, Karim alisema kuwa akiwa shambani hapo na mkewe pamoja na marafiki wengine wawili, watu hao waliotajwa kama wavamizi waliwafuata na kuwauliza walifuata nini shambani kwao huku wakiitana kwa miluzi, kitendo kilichowafanya waongezeke na kuwazunguka huku wakiwa na mapanga, fimbo na visu ambavyo vilitumika kuwapiga navyo.
 “Walikuwa si chini ya 30, walitupiga sana na mabapa ya mapanga wengine kutukata nayo baadaye wakapekua mifukoni na kutulazimisha kuwapa vitambulisho vyetu. Walitupokonya na fedha kiasi cha shilingi 780,000/=  ambazo zilikuwa nyumbani kwangu,” alidai Karim.
Naye mke wa Karim aliyejitambulisha kwa jina la Aisha Omary, alisema kuwa yeye na mfanyakazi wake walivamiwa wakiwa ndani ya nyumba yao iliyopo hukohuko shambani ambapo wavamizi hao walikuwa wakiongea Kikurya na kuwataka wafungue mlango ambao waliufungua baada ya kutishiwa kuuvunja.
“Baada ya kufungua walianza kutupiga kwa mabapa ya mapanga na mwenzangu walimkata mkono, wenyewe walidai shamba hilo ni la ndugu yao na siyo letu, nilipowabishia kwa ushahidi walizidi kutupiga na wakapekua na kutupokonya simu zetu na fedha tulizokuwa nazo, kama hiyo haitoshi walianza kutudhalilisha.
“Baadaye nilimuona mume wangu na wenzangu wakiletwa wakiwa wameloa damu. Wakasema watatuchoma moto na wakachukua petroli na kuanza kumwaga ndani, lakini rafiki yangu niliyeenda naye alikuwa ni Mkurya; akaanza kuwaomba kwa lugha ya kwao lakini hawakumuelewa,” alisema Aisha.
Aliongeza kuwa baadaye mmoja wao aliwaambia wenzake wawatoe nyumbani hapo na kuwataka wasirudi tena katika eneo hilo ndipo walikwenda Kituo cha Polisi cha Vikindu na kupewa hati ya kuwawezesha kutibiwa (PF3) na likafunguliwa jalada la kesi lililosomeka VK/RB/280/15 KUTISHIA KUUAWA KWA SILAHA na baadaye Kituo cha Polisi cha Mbagala, Kizuiani Dar ambapo walifungua jalada la kesi MBL/RB/3805/2015 KUJERUHI.
Akizungumza na waandishi wetu, Afisa iiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiio kwa tukio hilo na kuongeza:
 “Tayari jeshi la polisi limeshachukua hatua kwa kwenda eneo la tukio na hali ya eneo kwa sasa imekuwa shwari kwa kuwa kuna baadhi ya watu tayari wanashikiliwa wakihusishwa na tukio hilo.”

Post a Comment

Previous Post Next Post