TIKO AMEKIMBIA NYUMBA YAKE KISA MAMBO YA KISHIRIKINA

MWANADADA kutoka tasnia ya filamu na muziki Bongo, Tiko Hassan ameikimbia nyumba aliyokuwa akiishi maeneo ya Mwananyamala jijini Dar kutokana na mambo ya kishirikina.Akizungumza  hivi karibuni Tiko alisema kuwa, ameamua kuihama nyumba hiyo licha ya kwamba kodi yake haijaisha kufuatia maruweruwe yaliyokuwa yakimpata nyakati za usiku.
Mwanadada kutoka tasnia ya filamu na muziki Bongo, Tiko Hassan.
“Yaani nimekuwa nikishindwa kulala kwa raha kwani usiku huwa nasikia sauti za ajabu, mara nahisi kuna watu wanatembea ndani, mara mapaka yanalia dirishani kwangu, kimsingi sikuwa nikiishi kwa amani, nimeona nihamie Kinondoni yasije yakanikuta makubwa,” alisema Tiko

Post a Comment

Previous Post Next Post