Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Mh. Fadhil Nkurlu (kushoto) akimhoji dereva 
wa lori aliyejitambulisha kama Bw. Kabyemela (mwenye tisheti jekundu) 
baada ya kuwekewa mtego na kukamatwa na shehena ya ngozi ya magendo 
iliyokuwa ikisafirishwa kuelekea nchi jirani. Shehena hiyo ilikamatwa 
katika kizuizi cha Kyaka.

Baadhi
 ya ngozi ya magendo iliyokamatwa baada ya Mkuu huyo wa Wilaya kuweka 
mtego kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama. Shehena hiyo ya 
ngozi ya magendo inakisiwa kufika uzito wa takribani tani 10.
Mkuu
 wa Wilaya ya Missenyi Mh. Fadhil Nkurlu amekamata shehena kubwa ya 
ngozi ya magendo yenye uzito unaokisiwa tani 10 ikisafirishwa kwenda nje
 ya nchi bila kibali wala nyaraka zozote za serikali. 
Kutokana
 na taarifa za ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Missenyi ngozi hiyo ilitokea 
Kahama ikiwa inaelekea nchini Uganda na ilikamatwa katika kizuizi cha 
Kyaka, wilayani Missenyi. 
“Tulipata
 taarifa kutoka kwa raia wazalendo tangu jana yake kwamba kuna bidhaa za
 magendo ambayo huwa yanapita usiku, ndipo nikawapanga vijana kutoka 
vikosi vyote vya ulinzi na usalama kuweka mtego huu,” alisema DC Nkurlu.
“Hiki
 ni kipindi ambacho magendo ya kahawa husafirishwa kwa wingi kwenda nje 
ya nchi na hivyo hukosesha serikali mapato yake stahiki. Lakini 
tumejipanga ipasavyo na tutahakikisha tunakamata kila aina ya magendo. 
Hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakayejihusisha katika 
biashara hii,” alisisitiza.
“Napenda
 kutoa rai kwa wananchi wote wa Missenyi kuendelea kutoa ushirikiano wao
 kwa serikali ili kuweza kukamata bidhaa hizi za magendo na kudhibiti 
mtandao huu haramu,” alisema Mh. Nkurlu. 
Hii
 ni mara ya pili ndani ya wiki hii magendo yanakamatwa ambapo Jumatatu 
shehena kubwa ya mbao zilikuwa zikisafirishwa kinyemela zilikamatwa na 
bado zinashikiliwa katika kituo cha polisi cha Kyaka

Post a Comment