Picha
 ya Marehemu John Nyerere aliyefariki dunia juzi akiwa katika Hospitali 
ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa.
Marehemu
 John alizaliwa mwaka 1957 jijini Dar es Salaam na enzi za uhai wake 
alikuwa Kapteni wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) akiwa rubani wa 
kurusha ndege za kivita.
Kwa
 mujibu wa mmoja wa wanafamilia ni kwamba marehemu amefariki baada ya 
kusumbuliwa na maradhi ya mapafu na kisukari kwa muda mrefu.
Enzi za uhai wake John alishiriki vita ya kumng’oa Nduli Idd Amini nchini Uganda.
Mungu ailaze roho ya marehemu John mahali pema peponi. AMENI

Makamu
 Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula akisaini kitabu cha rambi rambi
 nyumbani kwa Baba wa Taifa Msasani jijini Dar es Salaam ambapo alifika 
kumpa pole Mama Maria Nyerere na familia yake kufuatia msiba wa mtoto wa
 Baba wa Taifa John Nyerere.

Makamu
 Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula akizungumza na Katibu wa 
Itikadi na Uenezi Nape Nnauye walipokutana nyumbani kwa Baba wa Taifa 
Msasani jijini Dar es Salaam kuhani msiba wa John Nyerere.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisaini kitabu cha rambirambi ya msiba wa John Nyerere.

Ndugu akitoa pole kwa Mama Maria Nyerere.

Katibu
 wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimpa mkono wa pole Mama Maria 
Nyerere kufuatia msiba wa mtoto wake John Nyerere kilichotokea juzi 
jijini Dar es salaam.

Katibu
 wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na Mama Maria Nyerere 
alipofika nyumbani kwake kumpa pole kufuatia msiba wa mtoto wake John 
Nyerere, wengine pichani ni Makongoro Nyerere (kushoto), Mwenezi wa CCM 
mkoa wa Dar es salaam Juma Simba Gadafi, na Anna Nyerere.

Katibu
 wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na Makongoro Nyerere 
Msasani nyumbani kwa Baba wa Taifa wakati wa kuhani msiba wa John 
Nyerere.(Picha zote na Adam Mzee).

Post a Comment