Mashambulio Yemen yawapa nguvu matakfiri Somalia

Ban Ki moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, uvamizi wa Saudi Arabia nchini Yemen umeyatia njia makundi ya kigaidi na kuyafanya yajizadidi na kushadidisha mashambulizi yao nchini Somalia. 

Ban amenukuliwa na shirika la habari la Associated Press akisema hayo jana katika ripoti yake kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kuongeza kuwa, usalama wa Somalia na eneo hilo zima la Pembe na Afrika na mashariki mwa bara hilo unatishiwa na uwepo wanamgambo wa ash Shabab wenye mfungamano na al Qaida. 

Matamshi hayo yamekuja katika hali ambayo tarehe 9 mwezi huu wa Mei, makundi ya kitakfiri yalitangaza kuhusika na mauaji ya Mbunge wa Puntland nchini Somalia, Said Hussein Nur, siku moja baada ya mbunge huyo kupigwa risasi na kundi la watu waliokuwa wamejizatiti kwa silaha wakati alipokuwa anatoka msikitini. 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amehusisha matukio hayo na mashambulizi ya Saudi Arabia nchini Yemen hususan kutokana na kuongezeka harakati za kigaidi za makundi ya kitakfiri nchini Somalia tangu Saudia ilipoanzisha mashambulizi dhidi ya wananchi wa Yemen. 

Nur ni mbunge wa pili wa Puntland kuuawa katika kipindi cha wiki chache zilizopita. Mwezi uliopita pia, wanamgambo wa ash Shabab walimuua kwa kumpifa risasi mbunge mwengine Aden Haji Hussein wakati alipokuwa ziarani mjini Mogadishu.

Post a Comment

Previous Post Next Post