Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki
ameteua timu ya wahandisi kutoka Wilaya za Temeke, Ilala na Kinondoni
kwa kushirikiana na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), kufanya
tathmini ya uharibifu wa miundombinu kutokana na mvua zinazoendelea
kunyesha pamoja na kujua gharama stahiki kulirudisha jiji katika hali
yake.
Akizungumza jijini jana, Sadiki alisema kuwa baada
ya kufanya tathmini hiyo, itatoa mwanga ni kiasi gani kinahitajika ili
kurudisha miundombinu iliyoharibika katika hali yake ya kawaida.
“Siwezi nikasema leo (jana) kuwa miundombinu
iliyoharibikia itafanyiwa matengenezo kwa kiasi hiki au kile, subirini.
Nimeitisha wahandisi na wanaendelea na kazi,” alisema Sadiki na kuongeza
kuwa;
“ Hiki kitu siyo cha kukurupuka kina taratibu na
sheria zake inabidi zifuatwe, hayo yote yakishakamilika wananchi wa mkoa
huu watafahamishwa lini ukarabati unaanza na kwa kiasi gani, kwani hapa
hakuna siri,”.
Akizungumza na gazeti hili juzi ofisini kwake,
mkuu huyo wa mkoa alisema mvua zimelivuruga jiji na kusababisha
uharibifu mkubwa wa miundombinu.
Sadiki aliyasema hayo baada ya kumalizika kikao
cha kutathmini mafuriko hayo kilichohusisha wakuu wa wilaya za mkoa huo,
Ilala, Kinondoni na Temeke, Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa na Kitengo
cha Maafa Mkoa.
Sadiki aliliambia gazeti hili kuwa, jiji haliko
kwenye hali nzuri kwani barabara zaidi ya 20 zimeharibiwa, madaraja
kadhaa, makaravati yamesombwa na maji na kusababisha kukatika kwa
mawasiliano katika baadhi ya maeneo.
Aliyataja maeneo yaliyoathirika zaidi kutokana na
mvua hizo ni pamoja na Keko, Chang’ombe Maduka Mawili, Yombo Vituka,
Vingunguti, Africana, Msasani Bonde la Mpunga, Jangwani, Manzese,
Kigogo, Mburahati, Boko na Basihaya.
Waathirika waweka ngumu
Licha ya kuathirika na mafuriko yaliyotokana na
mvua zilizoonyesha mfululizo kwa siku kadhaa, wakazi wa maeneo
yaliyopatwa na adha hiyo wamesisitiza kuwa hawatahama katika makazi yao
kwa sababu mafuriko yamewafuata.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili
walidai kuwa wameishi maeneo hayo kwa miaka mingi, wakipata huduma zote,
ikiwamo maji, umeme lakini hakukuwa na adha hiyo, huku wakiitupia
lawama Serikali kwa kushindwa kutafuta jinsi ya kuwasaidia.
Wakazi wa Magomeni Madaba ambako nyumba zilijaa
maji na kuonekana paa juzi na jana, kwa nyakati tofauti walisema kuwa
huu ni mwaka wa nne wanaingiliwa na maji na miaka minne iliyopita,
walipewa namba kwa ajili ya kupewa viwanja lakini hadi leo hawajapewa
Post a Comment