WOLPER ADAIWA KUPORA BWANA WA LUNGI, AJITETEA

Staa wa filamu za Kibongo, Lungi Maulanga amemshangaa msanii mwenzake Jacqueline Wolper kwa kutoka kimapenzi na mwanaume wake aitwaye Jimmy.

Jackline Wolper.
Sosi wa karibu na mastaa hao alidai kuwa, baada ya hivi karubuni gazeti ndugu na hili la Risasi Jumamosi kuandika kuwa Wolper amepata kigogo mpya aitwaye Jimmy, Lungi alishangaa, akajiuliza imekuwaje tena Wolper aamue kutembea na shemeji yake.
 

Jackline Wolper.

Ili kupata ubuyu uliokamilika, Lungi akasema: “Ni kweli Jimmy alikuwa mtu wangu, tukatofautiana kidogo, alipoenda Sauzi akakutana na Wolper ikadaiwa kuwa walitoka kimapenzi, nilishangaa kusikia hivyo na nimeamua kuachana na huyo Jimmy mwenyewe.
Wolper alipotafutwa kuzungumzia madai hayo alijitetea kwa kusema, yeye hajatoka na Jimmy ila walikutana tu Sauzi na kupeana kampani ya kawaida tu.

Post a Comment

Previous Post Next Post