KOCHA Mkuu waTaifa Stars , Mart
Nooij akisindikizwa kutoka uwanjani chini ya ulinzi mkali wa Polisi baada ya kumalizika
kwa mchezo wa timu yake na Uganda, Stars walilala kwa mabao 3-0,
Kamati ya Utendaji ya
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) katika
kikao chake cha leo
pamoja na mambo mengine kilipitia mwenendo wa timu ya
Taifa (Taifa Stars)
ikiwa ni pamoja na kuhudhuria mchezo kati ya Tanzania
na Uganda, kama sehemu
ya tathmini ya mwenendo wa timu.
*Kamati ya Utendaji kwa
kauli moja imeamua yafuatayo;*
*1. Ajira ya Kocha Mkuu
Maart Nooij inasitishwa mara moja kuanzia Juni 21,
2015.*
*2. Benchi lote la
ufundi la Taifa Stars limevunjwa kuanzia Juni 21, 2015.*
*3. Uongozi wa TFF
utatangaza punde benchi jipya la ufundi la timu ya
Taifa.*
*IMETOLEWA NA
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)*
Post a Comment