HII INASHTUA KIDOGO--KAULI YA ACT MUDA HUU DHIDI YA CHADEMA

WAKATI ikiwa imebaki miezi minne tu ili kufikia tarehe ya Uchaguzi mkuu wa Urais,wabunge pamoja na Madiwani hapo Octoba 25 mwaka huu,sasa Vyama vya Upinzani vya ACT-Wazalendo pamoja na Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema vimeingia tena kwenye  Uhasama mkubwa ambao unaweza ukavivuruga vyama hivyo.(Mtadandao huu unaripot)i.Anaandika KAROLI VINSENTendelea nayo

           Ni  Baada ya leo Chama cha ACT –wazalendo kusema wamepanga kukifanyia kitu kibaya chama cha Chadema ambapo wanadai Viongozi wa Chadema hawatakisahau maishani mwao.
         Hayo  yamesemwa Mda huu Jijini Dar Es Salaam  na Katibu wa  Mipango na Mikakati Taifa wa ACT-Wazalendo Habibu Mchange ,wakati wa mkutano na waandishi wa Habari ambapo Mchange amesema kwa sasa chama hicho kimechoka na kitendo wanachodai kinafanywa na Chadema cha kuwakodi watu kuja kufanya fujo kwenye mikutano yao.
       “ Sisi tumebaini wazi kwamba chadema wanawakodi watu na  kuja kufanya fujo kwenye mikutano yetu tumeona kule Tunduma mkoani mbeya na hata huyo Kionngozi wao Mnyika ametangaza kuwa sisi ni Adui basi wakiendelea ,tutawafanyi jambo baya sana na litakalokimaliza kabisa chama hicho,Amesema Mchange.
           Habibu Mchange ambaye anawania Ubunge kwenye Jimbo la Kibaha Mjini Mkoani Pwani kupitia chama hicho kwenye Uchaguzi mkuu wa hapo baadae mwaka huu  amebainisha kuwa  kwa kusema anaifahamu Chadema licha ya kuwa huko, kwani hawawezi kumtisha na atakavyowafanyia jambo baya hilo,anadai atatumia njia nyingi.
     “Mimi Chadema naijua kwani mimi ndio niliyoijenga chadema mpaka kufikia hapo,kama hamjui mimi ndio niliyotengeneza mipango kama ya  “Movement For Change” (M4C),Oparesheni Sangara,mimi ndio nilioijenga Chadema,kwahiyo hata hao wakina Dk Slaa na Mbowe wake hawawezi kufanya hivyo nawaambieni, hawezi kunipa shida kuwafanyia jambo baya,waendeleea waone”amebainisha Mchange..
               Wakati huo huo Chama cha ACT-Wazalendo kimewataka kupita viongozi wake, kimewataka Wananchi na wanachama wa chama hicho mkoani Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano mkubwa utakao fanyika Viwanja vya Mwembe Yanga vilivyopo Wilaya ya Temeke Mkoa wa Dar es Salaam siku ya Jumamosi ya Julai nne mwaka huu.

        Ambapo kwa mujibu wa Mchange amesema Mkutano huo mkubwa ambao utarushwa (live)yaani moja kwa moja kupita Vituo vya TV na Redio unatajwa kuwepo na Ajenda mbali mbali jambo analo anadai litakuwa linalengo la kumkomboa mtanzania wa leo.

Post a Comment

Previous Post Next Post