Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha ukombozi wa
Umma (CHAUMA) Hashim Rungwe akizungumza na waandishi wa habari wa Star
TV, TBC na ITV juu ya hali ya kampeni ilivyo hadi sasa.(PICHA NA HILLARY
SHOO).
Na Hillary Shoo, SINGIDA
ZIKIWA
zimebaki siku 27 kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu, Mgombea Urais wa
Tanzania kwa tiketi cha Chama cha Ukombozi wa Umma CHAUMA, Hashim
Rungwe, ametoa tathimini yake juu ya mwenendo wa kampeni pamoja na
matumaini yake katika kuibuka mshindi.
Rungwe
alisema ingawa ziko changamoto zinazojitokeza lakini kwa ujumla
kampeni zinakwenda vizuri na anamatumaini makubwa ya kuingia Ikulu
kutokana na watanzania kuhitaji mabadiliko.
Akiwa
Mkoani Singida ambao ni mkoa wa 10 katika mwendelezo wa ziara yake ya
kuwaomba Watanzania wamchague kuwa Rais, baada ya kumaliza mkutano wake
Mgombea huyo wa CHAUMA Hashim Rungwe alikutana na waandishi wa habari
kutoa tathimini juu ya mwenendo wa Kampeni.
Aidha
alisema kuwa Matumaini yake makubwa ni kuibuka mshindi na kuwa Rais
wa Tanzania katika awamu ya tano kwa kuwa wananchi wamechoka na ahadi za
kila siku kutoka chama tawala ambazo hazitekelezeki na huku maisha
yakizidi kuwa magumu.
“Huu
ni wakati sasa wa mabadiliko,tuwapumzishe hawa CCM wamechoka ,
wanatuita malofa na wapumbavu sasa ni wakati wa malofa na wapumbavu
kuongoza nchi hii, uwezo wao wa kuongoza ni mdogo, betri hazina chaji
wapuuzeni hawa, mimi betri ina chaji imejaa full, nipeni miaka mitano
muone kazi yangu.” Alisema.
Aidha
pamoja na matumaini aliyonayo, mgombea huyo anakiri kuwa mazoea na
umaarufu bado ni changamoto kubwa kwani watu wakisikia kuwa kuna mgombea
fulani wa chama watu wanajazana kuwasikiliza na wengine wanataka tu
kuwaona sura zao zikoje lakini ukweli unabaki kwenye mioyo yao.
“Mafuriko
kitu gani bwana wengine wanasikia tu fulani ni fisadi na hajawahi kuona
fisadi anafananaje na ndio maana wanafurika kwenye mikutano,hili mimi
halinitishi sera tu ndio jambo la maana kwangu na nina imani kubwa kuwa
nitaibuka kidedea. ‘ Alijigamba Rungwe.
Hata
hivyo Rungwe alisema kipindi alichokuja Papa John Paul II watu wengi
walijitokeza,wengine hata wasio Wakristo walifurika kumwona hata yeye
alikwenda kumwona, hivyo suala mafuriko kwake halimpi shida.
Ingawa
kila Mgombea wa Udiwani, Ubunge na Urais anamatumaini ya kushinda
katika uchaguzi mkuu, lakini jibu la ukweli linabaki kuwa kwenye
sanduku la kupigia kura siku ya Jumapili ya tarehe 25 mwezi ujao.
Post a Comment