Mzunguko
wa raundi ya sita ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania (VPL) unatarajiwa
kuendelea kesho Jumamosi na Jumapili kwa timu 10 kucheza kusaka alama 3
muhimu.
Jijini
Tanga Mgambo Shooting watakua wenyeji wa Coastal Union katika uwanja wa
Mkwakwani, Majimaji FC watawakaribisha Mwadui FC uwanja wa Majimaji
mjini Songea.
Jumapili
Stand United chama la wana watawakaribisha watoza ushuru wa jiji la
Mbeya (Mbeya City) katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, huku
Kagera Sugar wakiwa wenyeji wa Tanzania Prisons uwanja wa Ali Hassan
Mwinyi mjini Tabora na Toto Africa watakua wenyeji wa JKT Ruvu jijini
Mwanza uwanja wa CCM Kirumba.
|
Kikosi
cha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya
Kilimanjaro Premium Lager kimeanza mazoezi leo mchana katika uwanja wa
Taifa kujiandaa na mchezo dhdi ya Malawi utakaocheza Jumatano Oktoba 7,
2015 kuwania kufuzu kwa Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini
Urusi.
Stars
inayonolewa na kocha mkuu mzawa Charles Mkwasa, akisaidiwa na Hemed
Morroco, Peter Manyika na mshauri wa Ufundi Abdallah Kibadeni wameingia
kambini jana katika hoteli ya Urban Rose iliyopo Kisutu jijini Dar es
salaam.
Wachezaji
wote wameripoti kambini isipokuwa wachezaji wa kimataifa wanaocheza
soka la kulipwa nje ya nchi, Mrisho Ngasa, Mbwana Samata na Thomas
Ulimwengu wanaotarajiwa kuungana na wenzao mwishoni mwa wiki baada ya
kumaliza michezo inayowakabili wikiendi hii.
Wachezaji
waliopo kambini ni magolikipa All Mustafa, Aishi Manula, Said Mohamed,
walinzi Juma Abdul, Shomari Kapombe, Mohamed Hussein, Haji Mwinyi,
Hassan Isihaka, Kelvin Yondani na nahodha Nadir Haroub “Cannavaro”.
Wengine
ni viungo Himid Mao, Mudathir Yahya, Frank Domayo, Said Ndemla, Salum
Telela, Deus Kaseke, Saimon Msuva, Farid Musa, washambuliaji John Bocco,
Rashid Mandawa na Ibrahim Hajibu
|
Ligi
Daraja la Kwanza nchini (StarTimes First League) inaendelea wikiendi
hii kwa makundi yote matatu kucheza, michezo 11 itachezwa mwishoni mwa
wiki siku za Jumamos na Jumapili katika viwanja mbalimbali nchini.
Jumamosi
Kundi A, Ashanti United watakua wenyeji wa Mji Mkuu (CDA) katika uwanja
wa Karume jijini Dar es salaam, KMC watawakaribisha Polisi Dodoma
katika uwanja wa Mabatini – Mlandizi.
Kundi
B, Lipuli FC watawakaribisha Polisi Morogoro katika uwanja wa Wambi
mkoani Iringa, Kimondo FC watakuwa wenyeji wa JKT Mlale kwenye uwanja wa
CCM Vwava – Mbozi, huku Burkinafaso ya Morogoro ikiwakaribisha Njombe
Mji katika uwanja wa Jamhuri.
Kundi
C, JKT Kanembwa watakuwa wenyeji wa Panone FC katika uwanja wa Jamhuri
mjini Dodoma, JKT Oljoro watawakaribisha Polisi Moro uwanja wa Sheikh
Amri Abeid jijini Arusha, Geita Gold watacheza na Rhino Rangers uwanja
wa Nyankumbu mkoani Geita na Polisi Tabora watawakaribsiha Mbao FC mjini
Tabora uwanja wa Ali Hassa Mwinyi.
Ligi
hiyo itaendelea siku ya Jumapili kwa michezo miwili ya Kundi A, Friends
Rangers watacheza dhidi ya African Lyon uwanja wa Karume jijini Dar es
salaam, na Polisi Dar watakua wenyeji wa Kiluvya FC katika uwanja wa
Mabatini Mlandizi.
|
Rais
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu wa nchini (TFF), Jamal Malinzi ametuma
salam za pongezi kwa Alberto Simago Junior wa Shirikisho la Mpira wa
Miguu la Msumbiji (FMF) na Sidiki Tombi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu
nchini Cameroon (FECAFOOT) kufuatia kuchaguliwa kuwa marais wa
mashiriksho ya mpira miguu.
Katika
salam zake kwenda FMF na FECAFOOT, Malinzi amesema kuchaguliwa kwao
kuogoza mashirikisho hayo kumetokana na imani ya wanafamilia wa mpira
miguu.
Kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya TFF na familia ya mpira wa miguu nchini, anawapa pongezi kwa kucgahuliwa kwao.
TFF inaahidi kushirikiana na uongozi mpya wa FMF na FECFOOT katika maendeleo ya mpira wa miguu Afrika na Dunia kote.
|
Timu
ya Taifa ya Tanzania bara (Kilimanjaro Stars) imedhibitisha kushiriki
michuano ya timu za Taifa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA
Chalenjji) itakayofanyika nchini Ethiopia kuanzia Novemba 21 – 06
Disemba, 2015.
Michuano
ya CECAFA Chalenji ndio michuano mikongwe zaidi barani Afrika ambapo
jumla ya nchi 12 wanachama hushirki michuano hiyo iliyofanyika mara ya
mwisho mwaka juzi nchini Kenya na wenyeji kutwaa Ubingwa huo.
Nchi
wanachama wa CECAFA ni Tanzania Bara, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda,
Ethiopia, Eritrea, Djibouti, Somali, Sudan, Sudan Kusini na Zanzibar.
|
Post a Comment