Kiungo chipukizi wa Barcelona, Sergi Roberto
Kiungo chipukizi wa Barcelona, .
Na Rabi Hume
Kocha wa klabu ya Barcelona, Mhispania Luis Enrique amemtaja kiungo anayechupukia katika kikosi chake Sergi Roberto, 23 kama Zinedine Zidane mpya kutokana na aina ya uchezaji wake.
Enrique amesema hayo baada ya kumalizika kwa mchezo wa ligi kuu ya Hispania maarufu kama Primera Division uliyoikutanisha timu yake ya Barcelona na klabu ya Getafe na Barcelona kuibuka na ushindi wa goli 2 kwa bila, magoli yakifungwa na Luis Suarez na Neymar Jr.
Enrique amesema Roberto amekuwa na mchango mkubwa katika kikosi chake  kutokana na kutimiza majukumu anayokabidhiwa na mwalimu pamoja na aina yake ya uchezaji hali inayomfanya aone kama Zidane, Pele na Diedo Armando Maradona wakiwa ndani ya mtu mmoja ambaye ni mchezaji wake Roberto.
Kocha huyo  amemtaja Roberto kama aina ya mchezaji ambaye unaweza kumpanga kwa aina yoyote ya mfumo unaoutumia kama acheze kushoto, kulia au hata katikati na bado anazidi kuwa bora katika nafasi hizo.
Kocha wa Barcelona, Luis Enrique
Kocha wa Barcelona, Luis Enrique.
Aidha Enrique alimtaja kama Robert kama moja ya wachezaji wake bora kwa sasa katika kikosi chake kutokana na kuzungukwa na wachezaji bora wenye viwango bora duniani kama Sergio Busquets, Ivan Rakitic na Andres Iniesta.
“Amekuwa mchezaji mkubwa katika kikosi chetu cha Barca na amekuja na vitu vingi ambavyo vimefanya kikosi chetu kizidi kuwa bora pia kikichochewa na aina ya wachezaji wanaomzunguka Segio, Rakitic na Iniesta ambao wote wana uwezo bora zaidi,” alisema Enrique
Akizungumzia nafasi ya mchezaji huyo kwa siku za mbeleni amesema ataheshimu maamuzi yake lakini ni mchezaji muhimu kwa Barcelona.
Sergi Roberto ni moja ya wachezaji ambao wamekulia katika timu hiyo na mpaka sasa katika michezo 11 ambayo amepata nafasi ya kucheza amefanikiwa kutoa pasi za magoli 3 akilingana na Neymar pamoja na Lionel Messi ambaye kwa sasa ni majeruhi.