Kocha wa Klabu ya Chelsea, Jose Mourinho.
Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Brazil na klabu ya Chelsea, Oscar
Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Brazil na klabu ya Chelsea, Oscar.
Na Rabi Hume
Hali ya mabingwa watetezi wa kombe la ligi kuu ya nchini Uingereza, Klabu ya Chelsea sio nzuri kwa msimu wa 2015/2016 kufuatia kuanza msimu huu vibaya kwa kuambulia points 11 katika michezo 11 iliyocheza mpaka sasa na kukamatilia nafasi ya 15 hali ambayo inamuweka katika kipindi kigumu kocha wa timu hiyo, Mreno Jose Mourinho.
Hilo limethibitishwa na mshambuliaji wa timu ya taifa ya Brazil na klabu hiyo ya Chelsea, Oscar ambaye amesema hali ya kocha wake Mourinho imekuwa sio nzuri katika klabu hiyo kufuatia kipigo cha goli 3 kwa 1 walichokipata wikiendi hii dhidi ya mahasimu wao Liverpool mchezo uliochezwa katika uwanja wa Stamford Bridge.
Oscar amesema hayo wakati alipokuwa akizungumza na mtandao wa klabu ya Chelsea na kuelezea kuwa kabla ya mchezo huo wachezaji pamoja na mashabiki wa Chelsea walikuwa wakim-support kocha Mourinho lakini baada ya mchezo huo kumalizika hali imekuwa tofauti jambo lililofanya hali ya kocha huyo kuzidi kuwa mbaya ndani ya timu hiyo.
Mshambuliaji huyo ameongeza kuwa wachezaji wa timu hiyo pamoja na mashabiki wa timu hiyo wamekuwa wakijaribu kumsaidia kocha huyo ili kuweza kupata matokeo mazuri lakini matokeo yanakuja tofauti lakini wanachopaswa kufanya kwa sasa ni kupata matokeo mazuri.
“Kila mtu alijaribu kumsaidia (Mourinho) lakini hali sio nzuri kwa Mourinho kwa wachezaji na hata kwa mashabiki wa Chelsea, tunahitaji kuanza kushinda tena,” Oscar aliuambia mtandao huo.
Akiuzungumzia mchezo wa Liverpool Oscar amesema kuwa ulikuwa mchezo mzuri kwa upande wao katika kipindi cha kwanza lakini hali ilikuwa tofauti hasa baada ya mshambuliaji wa Liverpool, Phillipe Countinho kusawazisha goli la kwanza katika dakika za mwisho za kipindi cxha kwanza za mchezo huo.
Ameongeza kuwa katika kipindi cha pili wapinzani wao walikuja vizuri zaidi walijitahidi kuwazuia lakini walikuwa vizuri zaidi na kumwelezea, Mbrazil mwenzake anayekipiga Liverpool, Countinho kama nyota wa mchezo huo aliyefunga goli la pili kwa upande wa Liverpool kabla ya Christian Benteke kuongeza goli la 3 nala ushindi kwa Liverpool.