Msanii
supastaa wa muziki wa kizazi kipya anayeipeperusha vema bendera ya TZ
kimataifa, Diamond Platnumz, ameamua kuzungumzia ‘ishu’ ya uhalali wa mwanae
Tiffah.
Kwa muda
mrefu baadhi ya watu wamekuwa wakimpiga madogo Diamond kwa kusema Tiffah si
mwanae na wakaenda mbali zaidi kwa kumtaka akapimie DNA ili kupata ukweli.
Akizungumza
katika kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM, Jumatano usiku, Diamond akasema
hana mpango wa kupima DNA.
“Mimi ndio
nilipaswa kudai DNA, sio wao. Sina mpango wa kwenda kupima kwa sababu najiamini
mtoto ni wangu,” alisema Diamond.
Msanii huyo
akaongeza: “Hata kama mtoto si wangu au ni wangu, hiyo haiwahusu. Hebu tufanye
mambo ya kuleta maendeo badala ya vitu ambavyo havina msingi.
“Unamzungumzia
Tiffah ambaye anakuzidi kila kitu, Tiffah ni tajiri, anamiliki akaunti yenye
pesa nyingi, sasa inakusaidia nini kumzungumzia Tiffah.
Kuna watu
nimewakuta kwenye ‘game’ wamefanya muziki kwa muda mrefu lakini hawana
maendeleo yoyote kwasababu ya kuendekeza vitu ambavyo havina msingi.
“Watu
nimewazidi kila kitu, nimewazidi akili, nimewazidi uwezo wa kazi, sasa wanataka
kutafuta kick kupitia Tiffah.”
Chanzo: Saluti5
Post a Comment