MAJANGA! Bomoabomoa inayoendelea jijini Dar imemkumba msanii wa filamu, Wastara Juma aliyejikuta akizimia kwa mshtuko.
Ndugu
wa karibu wa mwigizaji huyo aliliambia Ijumaa kuwa hivi karibuni
Wastara aliwekewa alama ya X na maafisa wa ardhi katika nyumba zake
mbili zilizopo maeneo ya Tabata-Barakuda jijini Dar kuonesha kwamba ziko
kwenye eneo hatarishi.
STORI KAMILI
Ndugu huyo alizidi kudai
kuwa, siku maafisa hao walipokuwa wanaweka alama hiyo, Wastara hakuwepo
nyumbani na alipofika alishindwa kustahimili hali hiyo na kujikuta
akizimia na kuzinduka mara kadhaa.“Alipozinduka aliendelea kulia siku
nzima, anasikitisha kwa kweli,” alisema ndugu huyo wa karibu.
SIKU 10 ZAMPA MACHUNGU
Ndugu huyo aliendelea kusema kuwa kilichowashangaza ni kupewa siku kumi
za kuondoa vitu vyao hali inayowafanya wajiulize watavipeleka wapi
kwani siku ni chache.
“Unajua tumepatwa na mshtuko mkubwa kwani
hata hivyo tangu tuishi hapa hatujawahi kukumbwa na mafuriko ya aina
yoyote, ukiuliza ni kwa nini wameamua kufanya hivyo unaambiwa sehemu
hatarishi, kiukweli hatuna la kufanya tumechanganyikiwa,” alisema ndugu
huyo.
IJUMAA MZIGONI
Baada ya ndugu kuelezea tukio hilo, Ijumaa lilifunga safari hadi Tabata-Barakuda, zilipo nyumba zake hizo na kuzungumza naye.
ASHINDWA KUNYANYUKA
Waandishi walipotaka kuonana na Wastara kwa ajili ya mahojiano
kuhusiana na suala hilo alishindwa kunyanyuka kitandani hivyo kulazimika
kumfuata chumbani.
AFUNGUKA, AANGUA KILIO
“Sijui nina nini
jamani, serikali ingeniangalia ni juzi tu nimemaliza nyumba yangu, hapa
nilipo natafuta hela nyingi tu niende kwenye matibabu ya mguu wangu
sijapata linakuja hili ha! (analiaaa).
ATESWA NA FAMILIA
“Naifikiria sana familia yangu ni kubwa sijui nitaipeleka wapi na shida
niliyonayo nimechanganyikiwa, namuomba Mungu kiukweli,” alisema
Post a Comment