BAADA
ya Simba kuondolewa na Mtibwa kwenye mchezo wa jioni ya leo wa nusu
fainali ya kombe la Mapinduzi baada ya kufungwa bao 1-0, watani zao
Yanga nao wameondoshwa na URA kwenye michuano hiyo kwa changamoto ya
mikwaju ya penati 4-3
Yanga
ndio walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 13 kupitia kwa
Amissi Tambwe akimalizia kwa kichwa mpira uliotemwa na kipa Brian Bwete
kufuatia mpira wa kichwa uliopigwa na Simon Msuva.
Ikionekana
kama pambano hilo lingeisha ndani ya dakika 90 kwa Yanga kuibuka na
ushindi wa bao hilo moja, Peter Lwassa aliwainua vitini mashabiki wa URA
kwa bao safi la dakika ya 76 na kusababisha mechi hiyo iende kwenye
hatua ya penati.
Katika
hatua hiyo URA walifanikiwa kushinda kwa penati 4 dhidi ya 3 za Yanga.
Waliopata penati kwa upande wa Yanga ni Kelvin Yondan, Simon Msuva na
Deogratius Munishi 'Dida' huku Geofrey Mwashiuya na Malimi Busungu
penati zao zikiishia mikononi mwa kipa Brian Bwete.
URA
wao walipata penati zao kupitia kwa Jimmy Kulaba, Said Kiyeyu, Deo
Otieno na Bwete huku penati ya Sam Sekito ikiokolewa na Dida.
URA sasa watapambana na Mtibwa Sugar kwenye fainali itakayopigwa siku ya jumatano Januari 13 kwenye dimba hilo hilo la Amani.
Post a Comment