Model wa video ya ‘Kwetu’ alimtolea nje Abdu Kiba kuonekana kwenye Bayoyo

Abdu Kiba amesema wakati anafanya video yake mpya ya wimbo Bayoyo, alikutana na changamoto za hapa na pale moja ambayo iliyomsikitisha zaidi ni baada ya model aliyekuwa anatakiwa kufanya kutotokea na kutopokea simu zake katika hatua za mwisho.
Lyn 3
Hiyo ilimfanya kutafuta mbadala wa haraka.
“Unajua mrembo ambaye nilitakiwa kufanya naye video ni yule ambaye alifanya video ya Raymond ambaye nilipanga naye kila kitu hadi tarehe ya siku ya kusafiri kwenda kufanya video lakini baadaye simu huyo mrembo akawa hapokei na baadaye akazima simu,” Abdu alikiambia kipindi cha Clouds E.
Lyn 2
“Hiyo kwangu ilikuwa changamoto ambayo ilinitatiza sana na hiyo yote ni kwa sababu ya mambo ya team hizi ndio maana hakuweza kufanya video yangu ila siku ya siku ndio akapatikana model yule mwingine video ikafanyika.”

Post a Comment

Previous Post Next Post