DROGBA AHAMIA CHINA
Mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Didier Drogba (Pichani) ameingia mkataba na Klabu ya mpira wa miguu ya China ijulikanayo kama Shanghai Shenhua FC ya China, imefahamika kuwa Dgroga kasaini Mkataba wa miaka miwili na nusu na atajiunga rasmi na timu hiyo mwezi July mwaka huu, mkataba huo kati ya Drogba na Klabu hiyo unategemea kuisha mwishoni mwa mwaka 2014.
Kupitia Website yake Drogba alifunguka na kusema " Nimepokea mialiko mingi kwa wiki za hivi karibuni ila nimefikiri kuwa Shanghai
Shenhua FC ni timu nzuri ya kujiunga nayo kwa sasa, Ninatarajia
changamoto nyingi mpya ikiwemo kujifunza mila na desturi mpya, pia nina
shauku na maendeleo mapya katika mpira wa China"
Inasemekana
Drogba alitembelea nchi ya China mwaka jana na mapokeo yao yalikuwa
mazuri na kugundua kuwa na washabiki wengi. Drogba pia alisisitiza
kusaidia kukuza soka la China na kuhakikisha anatengeneza mahusiano
mazuri kati ya China na Afrika
Imefahamika kuwa Shanghai Shenhua FC inammiliki mchazaji mwingine wa zamani wa Chelsea anayejulikana na Nicolas Anelka.
Chanzo Habari
إرسال تعليق