Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi watoa maoni ya Katiba mpya

Mwakilishi wa Jimbo la Mji Mkongwe, Mhe. Ismail Jussa Ladhu akitoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya wakati wa mkutano uliotishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika ukumbi wa mikutano wa Baraza hilo jana Jumapili tarehe 14 Oktoba, 2012, ambao ulilenga kukusanya maoni ya Wajumbe hao kuhusu mchakato wa Mabadiliko ya Katiba Mpya.
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliotoa maoni yao yao mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba wametaka Zanzibar na Tanganyika ziwe na Mamlaka kamili huku mfumo wa muundo wa Muungano ukiwa wa mkataba…
Mwakilishi wa Jimbo la Mji Mkongwe,Ismail Jussa Ladhu alisema kwa mfumo wa muundo wa Muungano uliopo kamwe matatizo ya Muungano hayatasita hivyo ni lazima kubadili na kuwa na muundo wa mkataba ambao utakuwa ndio suluhisho la kero za Muungano.
Kwa mfumo huu tuliokuwa nao, idadi ya Serikali haziwezi kutatua kero ,katika matatizo haya sioni njia nyengine zaidi ya Muungano wa mkataba” Alisema Jussa.
Katika utangulizi wake,Jussa alisema tangu siku ya kwanza ya kuasisiwa kwa Muungano huu kulianza matatizo akitoa mfano kuwa wataalam waliotumika kuandaa  hati za Muungano hawakuwa Watanganyika wala Wazanzibari, ni raia wa Uingereza walioegemea zaidi kwenye mazingira ya nchi yao.
Mwakilishi wa Jimbo la Mwanakwerekwe(CCM),Shamsi Vuai Nahodha alipendekeza kuwepo na mabunge matatu chini ya mfumo wa muundo wa Muungano wa Serikali mbili, liwepo Baraza la Wawakilishi kwa ajili ya Zanzibar, Bunge la Jamhuri ya Muungano la wote  na liwepo Bunge dogo kwa ajili ya Tanganyika tu kwa mambo yasiyokuwa ya Muungano.
Shamsi ambaye pia ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa alipendekeza orodha ya mambo ya Muungano ipungue na akayataja mambo ambayo yanapaswa kubaki katika ushirikiano wa Muungano kuwa ni Ulinzi na Usalama, Uraia, Sarafu, Mambo ya Nje, Usalama wa Anga, Benki Kuu, mambo ya hali ya hatari, utabiri wa hali ya hewa na mengineyo.
Pia alipendekeza uhusiano wa kimataifa kila nchi iwe na mamlaka yake ya kusimamia eneo hilo sio kama ilivyo sasa ambapo mfumo uliopo sasa umekuwa na malalamiko ya muda mrefu.
Nae Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni(CCM), Salmin Awadhi Salmin alitaka  muundo wa sasa wa Muungano uendelee,lakini lazima Zanzibar iwe na mamlaka yake,suala la uhusiano wa kimataifa lisiwe la Muungano, Zanzibar iweze kuingia mikataba ya kimataifa, kujiunga na mashirika ya kimataifa kama OIC na mengineyo.
Muundo wa sasa wa Muungano uendelee,lakini katiba ieleze wazi mamlaka ya Zanzibar, Zanzibar iwe na mamlaka kamili katika Jamhuri ya Muungano …katiba hii ya sasa haizungumzi mgawanyo wa madaraka, pia katiba ieleze wazi zamu za Urais” Alisema Salmin.
Mwakilishi huyo aliongeza kwamba

Post a Comment

Previous Post Next Post