BREAKING NEWS - MSIBA: AHMED MGENI AFARIKI DUNIA LEO ZANZIBAR...




mgeni
 Muimbaji Nyota na mashuhuli, mwenye uwezo mkubwa wa kuimba AHMED MGENI wa Zanzibar Njema amefariki dunia leo alfajiri huko visiwani unguja. 

Muimbaji huyo ambae amekuwa akisumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu, alikuwa amelazwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar. 

Akizungumza na mtandao huu dada wa marehemu aitwae LAISATY MGENI alithibitisha ni kweli Kaka yake amefariki dunia leo alfajiri visiwani humo.

Ahmed Mgeni enzi za uhai wake aliwahi kupitia bendi kadhaa za taarabu ila wimbo wake wa SITETEREKI ndio umempa sifa sana.

AHMED MGENI atazikwa leo Saa kumi jioni sehemu iitwayo Amani Fresh njia ya Ziwatue huko huko visiwani Zanzibar.

Taarabu Zetu tunatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki kwa kuondokewa na kipenzi chetu Ahmed Mgeni na mungu amlaze pema peponi, AMIN!!

DOWNLOAD NA SIKILIZA NYIMBO YA "SITETEREKI" YAKE AHMED MGENI.. 

Post a Comment

أحدث أقدم