
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar 
Balozi Seif akimkabidhi zawadi Kipa Bora wa mashindano ya ujirani mwema 
ya Dr. Sheni Cup yaliyoandaliwa na Umoja wa Vijana wa CCM Jimbo la 
Nungwi.

 Balozi Seif akimkabidhi Kepteni wa Timu
 ya Soka ya Kitamli ya Nungwi Makame Mohd Haji jezi na vifaa baada ya 
timu hiyo kuibuka bingwa wa  Dr. Sheni Cup huko Nungwi Mkoa wa Kaskazini
 Unguja

 Balozi Seif akimkabidhi Kikombe Kepteni
 ya Mabanati wa Timu ya Pete ya Tusitengane ya Nungwi Ndamu Makame Mussa
 baada ya kuibuka na ushindi wa Kombe la Mwanamwema Sheni dhidi ya Timu 
ya Pete ya Tuko Imara.

 Kepteni wa Timu ya Soka ya Kitamli ya 
Nungwi Makame Mohd Haji akifuahia kikombe anachokabidhiwa na mgeni rasmi
 balozi Seif baada ya kutawadhwa kuwa mabingwa wa kombe hilo.
Kati kati yao ni lezi wa Jimbo la Nungwi Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa wa Idara Maalum Haji Omar Kheir.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar 
Balozi Seif akizungumza na Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Michezo 
Zanzibar { BTMZ } Sharifa Khamis hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar 
katyika kubadilishana mawazo ya namna ya kufufua michezo ya ndani 
inayoonekana mingi kufifia.
Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Michezo
 Zanzibar { BTMZ } Sharifa Khamis akipokea mchango wa shilingi Milioni 
2,000,000/- kutoka kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif 
Ali Iddi kwa ajili ya kusaidia ufufuaji wa michezo ya ndani inayoonekana
 kufifia hapa Nchini.
Picha na Hassan Issa wa – OPMR – ZNZ.
NA Othman Khamis Ame, OMPR
Hatimae Mabingwa wa 
Mashindano ya Ujirani mwema ya Dr. Sheni Cup yaliyoandaliwa na Umoja wa 
Vijana wa CCM Jimbo la Nungwi na kufadhiliwa na Rais wa Zanzibar Dr. 
Ali  Mohammed Sheni amepatikana katika mchezo wa Fainali ya mashindano 
hayo yaliyozikutanisha Timu za Soka za Kitamli ya Nungwi  dhidi ya 
wapinzani wao Timu ya Soka ya Mwendo Mdundo ya Kidoti.
Pambano hilo la 
Fainali lililoshuhudiwa na umati mkubwa wa wapenzi wa soka wa Jimbo la 
Nungwi na Vitongoji vyake limeiwezesha Wenyeji wa mashindano hayo Timu 
ya Kitamli ya Nungwi kuibuka na ushindi kwa kuilaza Mwendo Mdundo ya 
Kidoti Goli 1-0.
Timu ya Kitamli 
ilijipatia goli lake la pekee na la ushindi lililofungwa na mchezaji 
Haji Wa Haji katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo  ambapo mgeni 
rasmi katika pambano hilo la Fainali ya Dr. Sheni Cup alikuwa Makamu wa 
Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
Mashindano hayo ya 
ujirani mwema  yaliyoanza kutimua vumbi Tarehe 24/8/2013 yamejumuisha 
Timu  Tisa kutoka katika vijiji tofauti vya Jimbo la Nungwi yakienda 
sambamba na yale ya mchezo wa Pete { Net Ball } kwa Wanawake 
yaliyojumuisha Timu Nne.
Akizungumza mara baada
 ya pambano hilo la Fainali Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi 
Seif aliwahimiza Vijana hao kujitahidi kujifunza zaidi michezo ili 
wajijengee njia rahisi ya kupata ajira kupitia sekta ya michezo ambayo 
wakati huu imekuwa na thamani kubwa Duniani.
Balozi Seif alisema 
Ulimwengu hivi sasa umeshuhudia ongezeko kubwa la ajira kupitia Sekta ya
 michezo hasa Mchezo wa soka na Table Tennis ambayo imeonekana 
kutajirisha wanamichezo wengi wenye vipaji vikubwa vya michezo hiyo.
“ Tumeshuhudia 
wachezaji mbali mbali Duniani wakiwemo pia wale wanaotokea Bara letu la 
Afrika wakicheza mpira wa kulipwa katika timu mbali mbali za bara la 
Ulaya hasa ndani ya Uingereza. Huo ni Mfano halisi mmaopaswa kuutilia 
maanani ili na nyinyi siku moja mjikute mmetinga katika vilabu hivyo 
maarufu Duniani “. Alisisitiza Balozi Seif.
Mapema Mlezi wa Jimbo 
la Numngwi ambae pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na 
Idara Maalum Haji Omar Kheir alisema mashindano hayo yaliyoandaliwa na 
Umoja wa Vijana wa CCM wa Jimbo hilo kwa  ushauri wa Mke wa Makamu wa 
Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi ni utekelezaji wa Ilani
 ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2010.
Haji Omar alisema 
ilani hiyo imeeleza umuhimu wa uimarisha michezo katika maeneo mbali 
mbali nchini   lengo likiwa  kuwajengea afya njema pamoja na ajira 
wananchi wanaoshiriki michezo hiyo.
Katika kuunga mkono 
uendelevu wa mashindano hayo Waziri Haji Omar aliahidi kuchukuwa dhamana
 ya malipo kwa deni linalodaiwa Kamati ya mashindano hayo linalohusu 
malipo ya posho za waamuzi pamoja na baadhi ya vifaa vya mashindano 
hayo.
Katika fainali hiyo 
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alikabidhi Kikombe kwa 
Mabingwa wa Mashindano hayo Timu ya Kitamli ya Nungwi, Jezi, Mpira 
pamoja na Shilingi laki 300,000/-.
Balozi Seif pia 
alimkabidhi mshindi wa pili Mwendo Mdundo ya Kidoti Jezi, Mpira na 
Shilingi Laki 150,000/- wakati mshindi wa Tatu Timu ya Mapinduzi ya 
Kidagoni ikakabidhiwa  Jezi, Mpira na Shilingi 75,000/-.
Baadae Makamu wa Pili 
wa Rais wa Zanzibar akakabidhi shilingi 50,000/- kwa kila Timu bora , 
Mchezaji bora, mfungaji bora, Muamuzi bora, Mchezaji mdogo kuliko 
wote,kipa bora  pamoja na kocha bora kwenye mashindano hayo.
 Mashindano hayo 
yaliyopewa jina la Dr. Sheni Cup kwa mchezo wa Soka na Mwanamwema Sheni 
Cup kwa mchezo wa Pete { Net Ball } yamegharimu jumla ya shilingi 
milioni Sita Nukta Tano { 6,500,000/- }.
Wakati huo huo Makamu 
wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alikabidhi mchango wa shilingi 
Milioni 2,000,000/- kwa ajili ya kusaidia ufufuaji wa michezo ya ndani {
 Indo games } hapa Nchini ambayo mingi inaonekana kufifia na mengije 
kufa kabisa kwa  kipindi kirefu sasa.
Akikabidhi mchango huo
 kwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar  { BTMZ } Sharifa
 Khamis hapo Ofisini kwake vuga Mjini Zanzibar Balozi Seif alisema 
Zanzibar ilikuwa ikisifika kimataifa kwa michezo ya ndani sifa ambayo 
hivi sasa imekufa kutokana na kufifia kwa michezo hiyo.
Alisema juhudi za 
pamoja zinahitajika kuchukuliwa katika kuona michezo hiyo inachipuka 
tena hapa Nchini kwa kuwapa nguvu za uwezeshaji na vifaa wachezaji 
wanaojihusisha na  michezo hiyo.
“ Vijana lazima 
waendeleze pia michezo ya ndani kama vile Table Tennis, Vinyoya, Beach 
Ball, Triatholon na riadha badala ya kuelekezaa  nguvu zao zaidi kwenye 
soka ili kurejesha sifa hiyo Kimataifa “. Alisisitiza Balozi Seif.
Akipokea mchango huo 
Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar             { BTMZ } 
Sharifa Khamis { Sherry } alisema msaada huo wa Balozi Seif ni hatua ya 
awali katika kuunga mkono juhudi zinazochukuliwa na Taasisi za Michezo 
Nchini katika kufufua vuguvugu la michezo hapa Nchini.
Mwenyekiti Sharifa { 
Sherry } alisema katika kwenda samba mba na ufufuaji huo Baraza la Taifa
 la Michezo Zanzibar kwa kushirikiana na Chama cha Soka Zanzibar        {
 ZFA } hivi karibuni  vinatarajiwa kufungua vuguvugu la michezo katika 
kutimia miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964


إرسال تعليق