Kiwanda cha silaha uchochoroni chagundulika

POLISI mkoani Morogoro kwa kushirikiana na Kikosi cha kuzuia ujangili
kutoka Dar es salaam (KDU), wamegundua kiwanda kisichorasmi ‘bubu’
katika mtaa wa Kingo, Manispaa ya Morogoro ambacho kinatengeneza
silaha na nyingine kuzikarabati kinyume cha sheria.

Kufuatia kugundulika kwa kiwanda hicho, Polisi kwa kushirikiana na
Kikosi hicho wamekamata bunduki 11 na watu sita wakati watano
wanendelea kusakwa.

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro ,Faustine Shilogile alisema  , tukio
hilo lilitokea Septemba 14, maka huu  saa sita mchana katika mtaa huo
wa Kingo , Manispaa ya Morogoro .

Mbali na kushikilia silaha hizo, pia  watu sita  wanashikiliwa na
Jeshi hilo , wakati wengine watano wanatafutwa kutokana na kujihusisha
na kiwanda hicho.

Post a Comment

أحدث أقدم