NIMEANZA KUZOEA MAISHA YA MAN UNITED - FELAINI

 


Kiungo mpya wa Manchester United, Marouane Fellaini amesema sasa ameanza kuzoea mazingira.

Awali, Fellaini alilalama kwamba mazingira ya ugeni kuanzia mazoezini na hata sehemu anayoishi yalimpa mazingira magumu.
Fellaini ametokea katika mji wa Liverpool ambako ni makao makuu ya klabu ya Everton iliyomuuza man United kwa pauni milioni 27.



Lakini sasa, Fellaini anasema ameanza kuzoea mazingira na anaamini atafanya vizuri zaidi akiwa na kocha wake wa zamani David Moyes.


Bado Fellaini anaamini akiwa na wachezaji wengine kama Wayne Rooney, Robin van Persie, Michael Carrick, Ryan Giggs, Rio Ferdinand, Nemanja Vidic, Nani, Ashley Young, om Cleverley, atapata ushirikiano mkubwa.

Post a Comment

أحدث أقدم