GM watenga dola mil 300 kurejesha magari kiwandani kwa marekebisho


KAMPUNI ya magari ya General Motors (GM) ya nchini marekani inatarajiw akutumia zaidi ya dola za marekani milioni 300 katika robo ya kwanza ya mwaka kwa ajili ya kufanyia marekebisho ya magari yaliyokosewa kiufundi.
Kampuni hiyo imeyaita kiwandani magari milioni 1.5 klatika awamu tatu tofauti.
Wito huo mpya ni mbali na ule wa mwaka jana ambapo ulihusisha magari milioni 1.6 yaliyokosewa swichi za kuwashia.
Magari milioni 1.18 ni pamoja nay ale yaliyotengenezwa kati ya mwaka  2008 – 2013 aina ya  Buick Enclave na GMC Acadia; ya mwaka 2009 - 2013 aina ya Chevrolet Traverse na ya mwaka 2008 - 2010 aina ya Saturn Outlook, ambayo yalikuwa na matatizo na Maputo ya kujiokolea ya pembeni wakati wa ajali.
Pia kuna magari 303,000 aina ya Chevrolet Express na GMC Savana ya kuanzia mwaka 2009 - 2014 yakiwa na uzito wa pauni 10,000 au chini yaliyo na tatizo upande wake wa juu.
Aidha yapo magari 63,900 aina ya Cadillac XTS ya mwaka 2013 na 2014 yenye tatizo la joto na uwezekano wa kuzuka kwa moto katika injini na kuungua kwa vifaa vilivyotengenezwa kwa plastiki.
Taarifa zaidi zinasema kwamba kampuni hiyo ya GM  inakabiliwa na uchunguzi kwa namna ilivyoshughulikia kadhia hiyo ya kurejesha magari kiwandani yenye tatizo la swichi linazloweza kuzuia puito kufanyakazi yake wakati wa ajali.
Mtendaji mkuu wa kampuni hiyo Mary Barra amesema kwamba amewaambia wafanyakazi wa kampuni hiyo kuhakikisha kwamba wanafanyakazi kwa uaminifu nna kasi kurekebisha matatizo yaliyojitokeza.

Post a Comment

أحدث أقدم