MABAKI YALIYODAIWA KUONEKANA AUSTRALIA SI YA NDEGE YA MALAYSIA AIRLINES


March 20 2014 Waziri mkuu wa Australia alitangaza bungeni kwamba nchi yake kupitia picha za satellite imeona vipande kwenye bahari ya hindi ambavyo vinaaminika kuwa mabaki ya ndege ya Malaysia iliyopotea ikiwa na abiria 239 March 8 2014.

Saa kadhaa baada ya hizo taarifa kutoka, ilitangazwa kwamba vikosi vya uokoaji vimeshindwa kufika kwenye eneo hilo la tukio baharini kutokana na hali mbaya ya hewa iliyochangiwa na mvua.

Leo March 21 2014, taarifa kutoka vyombo vikubwa mbalimbali vya habari duniani, imefahamika hakuna kilichoonekana eneo la tukio kwenye bahari ya hindi ambako ‘ilisemekana’ vipande vya ndege hiyo iliyopotea vimeonekana hivyo vikosi vya uokoaji vimeondoka eneo hilo.

Post a Comment

أحدث أقدم