PICHA ZA TUKIO LA TUZO YA MWANAMAKUKA AWARDS 2014

Picha ya Kikundi, baadhi ya members wa UWF na  washindi wa miaka ya nyuma pamoja na Mshindi mpya wa Mwaka 2014 wakiwa katika picha ya pamoja.
Bi Jane Matinde, Ofisa wa maosiano wa Airtel, akikabidhi hundi ya udhamini ya million tano, kwa mwenyekiti wa UWF, Unity Of Women Friends Bi.Mariam Shamo,mwishoni Kulia ni Mkurugenzi wa benki ya Wanawake,Bi Magreth Chacha.Hafla hiyo iliofana kwa kiasi kikubwa ilifanyika kwenye kiota cha maraha cha Escape One,Mikocheni jijini Dar mwishoni mwa wiki.
Mshindi wa Awards 2014,Bi.Leila Mwambungu aangua kilio baada ya kutangazwa mshindi wa Tuzo ya Mwanamakuka.
Maryam Shamo, Mwenyekiti wa UWF na Meneja mradi wa Mwanamakuka, kulia na Mkurugenzi MKuu wa Benki ya Wanawake Tanzania,Bi.Magreth Chacha wakimkabidhi tuzo Mshindi wa mwaka 2014,Bi.Leila Mwambungu. 
Bi Magreth Chacha, Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Wanawake Tanzania,ambaye ni Mdhamini na Mdau mkubwa wa UWF katika kuwaongoza Washindi wa mwanamakuka katika kufikia malengo yao,akizungumza machache kwenye hafla hiyo.
 Mdhamini wa mradi wa Somki- Somesha Mtoto wa Kike top 15, Mr. Chriss Wade, akimkabidhi mmoja wa wahitimu aliyefanya vizuri katika mitihani yake ya kidato cha nne.
Picha Ya Pamoja, baadhi ya wanafunzi wanaonufaika na mradi wa Somesha Mtoto wa Kike, wakiwa na Members wa UWF na Mfadhili.
Dr.Vicensia Shule, mtaalam wa mambo ya ubunifu, akitoa mada kwa wanamakuka jinsi ya kuwa wabunifu kwenye kazi zao za mikono.
Mwana kikundi wa UWF ambaye pia ni Meneja mradi wa Somesha Mtoto Wa kike (SOMKI), Bi Belinda Ngowi, akielezea mafanikio makubwa ya mradi huo, haswa kwenye matokeo ya kidato cha nne wahitimu wote wamefanikiwa kupata daraja la kwanza na la pili.
Mwenyekiti wa UWF, Maryam Shamo akisema machache kuhusiana na mradi wa Mwanamakuka 2014.

Post a Comment

أحدث أقدم