Simba yapigwa 1 - 0 na Coastal, Azam nayo haishikiki


WEKUNDU wa Msimbazi, Simba wamejikuta wakiangukia pua mbele ya 'ndugu' zao kutoka Tanga, Coastal Union kwa kudunguliwa bao 1-0 na kuwafanya wapoteze matumaini ya kuendelea kuwepo kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu.
Simba, inayonolewa na kocha Zdrakov Logarusic, ilikumbana na kipigo hicho cha kushtukiza kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Bao pekee la mchezo ambao Coastal waliamua kuchezesha wachezaji wengi vijana badala ya wazoefu waliozoeleka, liliwekwa kimiani na Mohammed katika dakika ya45 Hamad Juma.
Simba pamoja na kucharuka kutaka kurejesha bao hilo ilijikuta ikishindwa kumtungia kipa Fikirini Suleiman.
Ushindi huo umekuja wakati Coastal ikitoka kupokea kipigo cha aibau cha mabao 4-0 toka kwa Azam na kujengeka hisia kwamba kuna hujuma iliyofanywa ndani ya kikosi hicho na ndicho kinachoelezwa kimemfanya kocha Yusuph Chipo kufanya mabadiliko katika kikosi chake kilichoivaa Simba.
Katika mechi nyingine, Azam imeendelea kuonyesha dhamira yao ya kutwaa ubingwa msimu baada ya kuinyuka Oljoro JKT kwa bao 1-0, bao lililofungwa na John Bocco 'Adebayor' katika dakika ya 71.
Mechi hiyo ilichezwa kwenye uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam na kuifanya Azam kufikisha pointi 47 nne zaidi na ilizonazo Yanga ambayo haya hivyo ina mchezo mmoja mkononi.
Kwa kuinyuka Simba, mabingwa hao wa Tanzania wamefikisha pointi 29, huku Simba wakisaliwa na pointi 36 wakisalia nafasi ya nne.

Post a Comment

أحدث أقدم