Vikwazo kwa mazoezi Bujumbura

Barabara za mji wa Bujumbura
Mji mkuu wa Burundi, Bujumbura umekua na sifa ya kuwa na wakaazi wengi wanao fanya mazoezi ya mwili na hasa mwishoni mwa wiki ambapo barabara zote hujaa makundi ya watu wanaotembea au kukimbia.
Lakini kwa sasa yote hayo hayatofanyika bila kupata ruhsa maalum kutoka manispaa ya jiji. Watu wengi wanaopenda kufanya mazoez wanalalamika kuwa uhuru wao umekandamizwa.
Meya wa jiji la Bujumbura Said Juma, ametoa amri inayokataza watu kufanya mazoezi wakiwa wengi kwenye barabara za Bujumbura.
Meya amesema baadhi ya vyama au mashirika ya kisiasa yanatumia fursa ya kujikusanya kwenye michezo na mazoezi ya pamoja ili kuandaa maandamano au kuchochea ghasia na vurugu kwenye barabara mbali mbali kwa ukiukwaji sheria.
Wapenzi wa mazoezi wanasema huu ni ukandamizaji
Mwandishi wa BBC mjini Bujumbura Ismail Misigaro, anasema kuwa hatua ya kwanza ni mazoezi yalokuwa yakifanywa kila Jumamosi yamefutwa kabisa.
Ni marufuku watu kufanya mazoezi ya watu wengi barabarani badala yake imeruhusiwa kufanya mazoezi hayo katika maeneo maalum yanayoruhusiwa kufanyia michezo na mazoezi.
Katika taarifa hiyo Meya Said Juma amevitaja viwanja karibu tisa vya soka mjini Bujumbura kama maeneo yanayo ruhusiwa watu kufanya mazoezi wakiwa pamoja au kwa wingi.
Amri hii imetolewa baada ya purukushani iliyojitokeza mapema mwezi huu baina ya chama cha upinzani cha MSD na polisi ambapo zaidi ya wafuasi 50 wamefungwa jela maisha.

Post a Comment

Previous Post Next Post