Diamond na Mzee Yusuf kuumana Dar Live

http://photos-b.ak.instagram.com/hphotos-ak-xfa1/t51.2885-15/10838471_1574256322809473_1640804524_n.jpgDar es Salaam. Wapenzi wa burudani ya muziki wa kizazi kipya na muziki wa taarabu watapata burudani ya funga mwaka kutoka kwa gwiji wa muziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz na mfalme wa muziki wa taarabu, Mzee Yusuf watapanda jukwaa moja katika ‘Tamasha Wafalme’ litakalofanyika katika Ukumbi wa Dar Live, Mbagala.
Tamasha hilo la wafalme ambalo limeanza kuwa gumzo la jiji kutokana na kuwa na burudani za aina mbalimbali kwa ajili ya kukonga nyoyo za wapenzi wa burudani limedhaminiwa na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania.
Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu alisema Vodacom imeamua kudhamini tamasha hilo kwa ajili ya kuwapatia furaha na burudani wateja wake na wananchi kwa ujumla katika msimu huu wa sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya.
“Kama ilivyo kaulimbiu yetu kuwa ‘ukiwa na Vodacom maisha ni murua’, tunahakikisha mbali na kutoa huduma bora kwa wateja wetu pia tunajua kuwa kuna muda wanahitaji kufurahi kwa burudani, hivyo ndiyo maana tunadhamini matamasha ya aina hii na tutaendelea kufanya hivyo siku zote.”

Post a Comment

Previous Post Next Post