Nyota hawa Simba, Yanga kwisha


Dar es Salaam. Klabu za Simba na Yanga zimefanya mabadiliko kwenye vikosi vyao na moja kwa moja watakuwa wameathiri nafasi za baadhi ya wachezaji wa vikosi hivyo.
Timu zote hizo kongwe zimefanya mabadiliko zaidi katika kujiimarisha lakini pamoja na mapendekezo mapya yaliyowekwa, imewaweka pabaya baadhi ya wachezaji na hivyo kufanya wakati wao kuwa mgumu.
Yanga imewasajili Mliberia Kpah Sherman, Mrundi Amissi Tambwe na Danny Mrwanda kwenye safu ya ushambuliaji na kipa Athumani Majogo, wakati Simba imewasajili Dan na Simon Sserunkuma, Juku Musheed (wote raia wa Uganda) na Hassan Kessy. Wafuatao watakalia kuti kavu Simba kipindi hiki;
William Lucian ‘Gallas’
Usajili wa Hassan Kessy aliyetokea Mtibwa Sugar utampa wakati mgumu beki huyu na kwamba anaweza kuwa chaguo la pili kama si la tatu. Licha ya kuwa na uzoefu na umri wake bado ukiwa mdogo, Lucian atakuwa na wakati mgumu wa kupata nafasi mbele ya Kessy, ambaye amekuwa akiwindwa na Simba kwa kipindi kirefu bila mafanikio hapo awali.
Nassor Masoud ‘Chollo’
Beki huyu mkongwe wa Simba ameonekana kurudisha makali yake hivi karibuni, lakini inasadikiwa uwepo Kessy utamrudisha tena benchi.
Chollo hajawa na kipindi kizuri kwa takribani mwaka sasa kutokana na matatizo ya majeraha. Chollo uenda akawa mbadala wa Kessy kwenye kikosi cha kwanza cha Simba.
Hassan Isihaka:
Hakika amekuwa akifanya kazi kubwa na hata kuaminika kuanza kwenye michezo yote ya kirafiki na ya ligi kwa msimu huu. Isihaka amekuwa akicheza sambamba na Joseph Owino lakini hali ilivyo sasa baada ya usajili wa beki Juku Musheed, huenda akapoteza nafasi.
Shaban Kisiga ‘Marlone’
Licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kuichezesha timu na kufunga mipira ya faulo. Kiungo huyo mshambuliaji anaweza kupoteza nafasi kwa washambuliaji Dani Sserunkuma na Elius Maguli ambao ni chaguo la kwanza la Kocha wa Simba Patrick Phiri aliyetokea kwenye klabu ya Gor Mahia ya Kenya.
- Mwananchi

Post a Comment

Previous Post Next Post