Waislamu
wa madhehebu ya Shia nchini wamempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa
kumtimua Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna
Tibaijuka pamoja na kumsimamisha kazi Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati
na Madini, Eliakim Maswi, kupisha uchunguzi kuhusu sakata la akaunti
ya Tegeta Escrow.
Pongezi hizo zimetolewa Jana na Imamu wa Msikiti wa Mashia wa Kigogo, Dar es Salaam, Sheikh Hemed Jalala , wakati akitoa salamu za sikukuu ya Krismas kwa Wakristo nchini na Duniani nakuwatakia kheri ya Mwaka Mpya wa 2015.
Alisema lengo la salamu hizo ni kuonyesha kuwa waumini wa dini ya Kiislamu na Wakristo wapo pamoja na kushirikiana katika mambo mbalimbali ya kimaendeleo na furaha.
“Waislamu wana itikadi zao pia Wakristo, hivyo hivyo, kinachotuunganisha sisi ni utaifa tulionao ambao unapelekea kuvumiliana katika mambo mengi,” alisema Shekhe Jalala.
Alisema Serikali inapaswa kuwaangalia kwa karibu viongozi wa dini zote nchini kama ni watu ambao wataendeleza umoja uliopo na kudumisha amani iliyopo.
“Endapo amani na umoja vikitoweka nchini hakuna kiongozi wa dini ambaye ataweza kukaa katika nyumba ya ibada na kuhubiri amani tena kama ilivyo sasa ,” alisema.
Pongezi hizo zimetolewa Jana na Imamu wa Msikiti wa Mashia wa Kigogo, Dar es Salaam, Sheikh Hemed Jalala , wakati akitoa salamu za sikukuu ya Krismas kwa Wakristo nchini na Duniani nakuwatakia kheri ya Mwaka Mpya wa 2015.
Alisema lengo la salamu hizo ni kuonyesha kuwa waumini wa dini ya Kiislamu na Wakristo wapo pamoja na kushirikiana katika mambo mbalimbali ya kimaendeleo na furaha.
“Waislamu wana itikadi zao pia Wakristo, hivyo hivyo, kinachotuunganisha sisi ni utaifa tulionao ambao unapelekea kuvumiliana katika mambo mengi,” alisema Shekhe Jalala.
Alisema Serikali inapaswa kuwaangalia kwa karibu viongozi wa dini zote nchini kama ni watu ambao wataendeleza umoja uliopo na kudumisha amani iliyopo.
“Endapo amani na umoja vikitoweka nchini hakuna kiongozi wa dini ambaye ataweza kukaa katika nyumba ya ibada na kuhubiri amani tena kama ilivyo sasa ,” alisema.
CHANZO:
NIPASHE
Post a Comment