WASANII WATATU WA BENDI YA SUPER STAR YA MWANZA WAFUNGWA MIEZI 14 JELA KWA KOSA LA KUINGIA NCHINI BILA KIBALI.


IDARA ya Uhamiaji mkoani Geita imewaonya wamiliki wa kumbi za starehe kuacha kuajili wasanii kutoka nje ya nchi bila kufuata taratibu za uhamiaji hali ambayo ni kinyume cha sheria za nchi.
Onyo hilo limetolewa leo na Mkuu wa uhamiaji mkoa wa Geita,Kamishina Msaidizi Mwandamizi,Charles Washima,wakati akiongea na kipindi hiki mara baada ya kubaini baadhi ya wasanii katika kumbi hizo ni raia wan chi za nje.
Washima amesema wiki iliyopita idara yake imewakamata wasanii watatu wa bendi ya Super star ya jijini Mwanza wakiwa Raia wa Nchi ya Kongo ambao walikuwa wakifanya kazi za muziki bila kibali.
Aidha Washima amesema kufanya hivyo ni kinyume cha taratibu na watu hao tayari wamehukumiwa mahakamani vifungo vya miezi kumi na nne kila mmoja,na kulipa faini ya Shilingi Laki Moja kwa kila mmoja.
Amesema kufuatia hali hiyo wamiliki wa kumbi za starehe wanapaswa kufuata sheria kuliko kuajiri wasanii kutoka nchi za nje bila kibali hali ambayo hata wamiliki wenyewe idara yake itawachukulia hatua za kisheria.
Amewataja wasanii waliokamatwa na idara yake na kisha kufungwa jela ni pamoja na Mpiga gitaa wa bendi wa Super Star,Kashindye Byamungu{18},Dhahiri Kwamlima{22}mwimbaji pamoja na Edward Wamwamba{25}Mwimbaji wote raia wa nchi ya Kongo.

Post a Comment

أحدث أقدم