
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
akiwapungia wananchi wakati alipokuwa akiingia katika uwanja wa Uhuru
jijini Dar es salaam kuongoza maadhimisho ya mika 48 ya Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar leo asubuhi.
Amiri jeshi
Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua vikosi vya ulinzi na
usalama wakati wa maadhimisho ya sikukuu ya miaka 48 ya Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya
Viongozi wa Kiserikali wakiwa ni miongoni mwa waliohudhuria sherehe hizo
katika Uwanja wa Uhuru, wakisimama wakati wa kumkaribisha Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais Jakaya
Kikwete, akisalimiana na Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati
akiwasili kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo Aprili 26,
2012 katika sherehe za maadhimisho ya miaka 48 ya Uhuru wa Tanganyika na
Zanzibar.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mama Maria Nyerere leo katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa CUF Profesa
Ibrahim Lipumba wakati alipowasili katika uwanja wa Uhuru kuongoza
sherehe za Muungano zilizofanyika leo jijini Dar es salaam.
Vikosi vya
Ulinzi na Usalama vikipita na kutoa heshima mbele ya jukwaa kuu kwa
mwendo wa pole na haraka, wakati wa maadhimisho ya sherehe hizo leo.
Watoto wa
shule mbalimbali za msingi wanaounda kikundi cha alaiki, wakionyesha
manjonjo ya michezo na maumbo mbalimbali wakati wa sherehe hizo leo.
Kikundi cha Sanaa cha JKT Oljoro, kikionyesha umahiri wake wa kuimba na kucheza ‘Kiduku’ wakati wa sherehe hizo. (picha zote na Freddy Maro,Muhidin Sufiani)
Chanzo:- Mo blog












إرسال تعليق