RC MBEYA AAGIZA MTU ALIYEGUSHI BARUA KUTOKA OFISI YA WAZIRI MKUU AKAMATWE
Hii ndiyo barua iliyogushiwa |
“Hili
ni kosa kubwa kwa mtu kuibuka na kutoa vitisho kwa kutumia majina ya
viongozi wa juu na ofisi zao, kwani tumefanya uchunguzi wa barua hizo
kwanza hazijafuata taratibu za serikali, lakini pia wahusika waliotajwa
kutoa barua hiyo toka TAMISEMI wamekataa kuhusika tena kwa maandishi.”
Alisema Kandoro.
Alitumia
fursa hiyo kuonyesha na kugawa nakala za barua hiyo kwa waandishi wa
habari, yenye kumbukumbu namba CAB.65/223/01/23 iliyoandikwa na Katibu
Mkuu wa TAMISEMI M.A Pawaga, ikiwa na baadhi ya maneno yanayosomeka .
… “Kama ulivyoitilia mashaka barua hiyo na tathmini iliyofanywa
ofisi hii hasa kwa kuzingatia saini ya mwandishi pamoja na mtiririko
wa maudhui ya barua hii, tumegundua kuwa ni ya kughushi ,” ilifafanua
sehemu ya barua hiyo
Akifafanua
zaidi kuhusu zhilo Kandoro alisema hakuna sehemu wala kipengele kwenye
sheria ya kahawa kinachozungumzia biashara ya kahawa mbichi, hivyo
kitendo cha watu kutaka kulazimisha biashara hiyo ni makosa kisheria.
Hata
hivyo Kandoro alipobanwa aeleze uchgunguzi wa awali umebaini mhusika
aliyeandika barua hiyo, alisema suala hilo ni la kitaalamu na tayari
rimeshafikishwa polisi wao ndio wanauwezo wa kumbaini mhusika na
hatimaye kumkamata.
Wakati
mkuu wa mkoa akitoa agizo hilo, kanda wa polisi mkoani hapa Advocate
Nyombi alipoulizwa hatua zilizofikiwa alidai yuko likizo, lakini baadhi
ya maofisa wa jeshi hilo ambao si wasemaji walilihaskikishia gazeti
hili kuwa suala hilo lipo mikononi mwa polisi na linafanyiwa kazi
.
Hata
hivyo hawakuwa tayari kueleza kama mhusika amekamatwa na kuwataka
waandishi kuwa na subira ili uchunguzi ukamilike na hatua zitakazokuwa
zimechukuliwa juu ya sakata hilo la kughushi nyaraka muhimu za serikali
.
Sakata
la ununuzi wa Kahawa mbichi wilayani Mbozi limekuwa la muda mrefu
ambapo baadhi ya kampuni zilizopigwa marufuku na serikali ya mkoa
kulalamika kuwa uamuzi huo ni wa kibabe kwa kuwa wao wananyaraka
halali za serikali zinazowaruhusu kununua kahawa hiyo.
Miongoni
mwa kampuni hizo ni Lima ltd , ambayo inadaiwa kughushi barua yenye
kumbukumbu namba A.1 80/361/12/09,inayodaiwa kuandikwa na mmoja wa
maofisa waandamizi kutoka ofisi ya Waziri mkuu aliyetajwa kwa jina la
D. Bandisa,ikimtaka Mkuu wa Mkoa kwa kushirikiana na uongozi wa wilaya
ya Mbozi kuiruhusu kampuni hiyo kuendelea na ununuzi wa kahawa
mbichiwilayani humo.
Lakini
miaka miwili iliyoipita madiwani kutoka halmashauri zote zinazolima
zao hilo zilipinga uuzaji wa kahawa mbichi kupitia vikao vya baraza la
madiwani.
Habari kwa hisani ya Kenneth Ngelesi, Mbeya
Picha na Josep Mwaisango
Picha na Josep Mwaisango
Post a Comment