UTEUZI WA WAKUU WA WILAYA WAKAMILIKA WANAHABARI WAULA ,MADC 51 WATEMWA


 UTEUZI WA WAKUU WA WILAYA WAKAMILIKA WANAHABARI WAULA ,MADC 51 WATEMWA



Waziri Mkuu Mheshimiwa MIZENGO PINDA ametangaza Wakuu wapya wa Wilaya huku Wakuu wa Wilaya 51wa zamani akiwaacha kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya kustaafu kazi.
Akitangaza Wakuu hao wapya wa Wilaya mbele ya Wahariri wa vyombo vya habari nchini, Waziri Mkuu amesema kati ya Wakuu hao wa Wilaya 133 walioteuliwa wapya ni Sabini wakiwemo Waandishi wa habari Sita.

Kulingana na Waziri Mkuu kabla ya kutangazwa kwa Wilaya mpya kulikuwa na Wakuu wa Wilaya 114 ambapo kati ya Wakuu hao wa Wilaya wa Zamani 63 wamebaki katika uteuzi wa leo na 51 wameachishwa kazi.

mkuu wa wilaya mkoa wa Mbeya aliyetangaza kujiuzulu atemwa rasmi
 Habari zaidi zitawajia yakiwemo na majina ya wakuu hao wa Wilaya.

Post a Comment

Previous Post Next Post