AZAM IKO TAYARI KUWAPA YANGA SURE BOY JR.
Sure Boy Je kazini Azam |
UONGOZI wa klabu ya Azam FC umeipa ruhusa Yanga kuwasilisha
ombi la kumsajili kiungo, Salum Abubakar ‘Sure Boy Jr.’, lakini tu waende na
ofa ya kueleweka.
Meneja wa Azam FC, Patrick Kahamele amesema mchana huu
kwamba, sera ya Azam si kuwazuia wachezaji wanaotaka kuondoka, lakini wanataka
taratibu zifuatwe.
“Yanga kama wanamtaka Sure Boy walete barua rasmi ya maombi,
tena waje na ofa ya maana, tutawauzia,”alisema Kahamele.
Sure Boy Jr. aliyeng’ara kwenye mechi ya Taifa Stars na Gambia
Jumapili, Uwanja wa Taifa, akicheza kwa uelewano mkubwa na Frank Damayo na
Mwinyi Kazimoto katika safu ya kiungo, ni mtoto wa kiungo wa zamani wa Yanga,
Abubakar Salum ‘Sure Boy’.
Mwaka jana, Yanga
waliomba kumsajili Mrisho Ngassa kutoka Azam, lakini wakakwama kutoka dau lao
dogo, Sh. Milioni 25. Azam pia imesema hata Ngassa wako tayari kumuacha aende
Yanga, iwapo watatoa ofa nzuri.
Post a Comment