KAMATI ya Bunge ya Mashirika ya Umma (POAC), imelazimika
kuwarudisha wajumbe wa bodi ya Shirika la Viwango Nchi
ni (TBS) kutokana
na maswali ya ukaguzi 13 kushindwa kupatiwa ufumbuzi.
ni (TBS) kutokana
na maswali ya ukaguzi 13 kushindwa kupatiwa ufumbuzi.
Licha ya hayo pia wameitaka bodi hiyo kuja na majibu na mapendekezo
yao juu ya ukaguzi maalumu uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na uchunguzi uliofanywa na kamati ndogo
ulioongozwa na Deo Filikunjombe kuhusu mawakala wa ukaguzi wa magari wa
Hongkong na Singapore.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam,
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Zitto Kabwe (Chadema), alisema kuwa kutokana
na kupitia taarifa hiyo wamebaini upungufu hivyo kamati yake imeagiza
bodi hiyo ikajipange upya na kuja na taarifa sahihi.
Akitolea mfano alisema kuna suala la wakala wa ukaguzi wa magari
yanayoingia nchini ambapo wamekuwa wakifanya kazi bila kuwa na leseni
hatua ambayo inaiwia vigumu serikali kupata fedha inazodai kutoka kwa
mawakala hao kiasi cha dola milioni 253.
Zitto ambaye ni mbunge wa Kigoma Kaskazini alisema pamoja na shirika
hilo kutakiwa kufanya ukaguzi wa bidhaa mbalimbali lakini wameshindwa
kufanya kazi hiyo na matokeo yake kumekuwepo na bidhaa zisizo na ubora
kuingia nchini.
“Kuna bidhaa ambazo taarifa ya CAG imezigundua kuwa hazifai kwa
matumizi ya binadamu kama vile omo, mafuta ya magari, matairi, mbolea
lakini zimekuwa zikiingizwa kwa kibali cha Mkurugenzi Mkuu wa TBS
Charles Ekelege,” alisema.
Zitto alisema bidhaa nyingi ambazo ni bandia zilioneshwa kukaguliwa na
kugundulika ubovu wake, lakini zimeendelea kutumika kutokana na wenye
kampuni hizo kufanya mawasiliano na Ekelege naye kutoa kibali cha
kuingizwa kwa bidhaa hizo.
Zitto alisema kuwa bodi hiyo inapaswa kuja na mapendekezo mapya Juni
30, mwaka huu, huku wakitakiwa kufanya kazi zao kwa umakini kuhakikisha
wanatimiza wajibu wao kwa kuteketeza bidhaa bandia.
إرسال تعليق