Mwape atupiwa virago Jangwani
UONGOZI wa klabu ya Yanga umesitisha rasmi mkataba wake na
mshambuliaji wao wa kimataifa, Devis Mwape huku vifaa vyao vipya vya
kimataifa vikitua klabuni hapo leo kwa ajili ya maandalizi ya Kombe la
Kagame, michuano inayoanza kutimua vumbi Julai 14 jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mkuu wa klabu hiyo, Celestine Mwesigwa alisema wameamua kuachana na
mchezaji huyo na kumuongezea mkataba beki Shadrack Nsajigwa kutokana na
uzoefu wake kwenye klabu hiyo.
Nsajigwa alielezwa kujiunga na Gor Mahia ya Kenya baada ya kuwapo taarifa kuwa alikuwa na mpango wa kuachwa katika klabu hiyo.
Katibu
wa Wazee wa Yanga, Ibrahim Akilimali alisema klabu yao mwaka huu
imeamua kusajili wachezaji chipukizi wenye uwezo. Alisema pia kuwa
wachezaji wa nje wameshamalizana.
Awali ililipotiwa kuwa wachezaji ambao wanatarajia kuachwa ni Mwape, Yaw Berko na Kenneth Asamoah.
Yanga imeanza mazoezi jana chini ya kocha wao msaidizi Felix Minziro kwa ajili ya Michuano ya Kagame.
Yanga imeanza mazoezi jana chini ya kocha wao msaidizi Felix Minziro kwa ajili ya Michuano ya Kagame.
Post a Comment