WALIOUA SIMBA HAWA 6 ‘NAIROBI NATIONAL PARK’ KUPAMBANA NA MKONO WA SHERIA.

Polisi na mamlaka ya wanyama pori nchini Kenya wapo katika msako mkali kuwatafuta wakazi wa Kitengela walioua simba sita kutoka hifadhi ya taifa ya Nairobi.
Simba hao wanaodaiwa kuvamia na kuua kondoo 28 siku ya jumatono asubuhi.
Mkurugenzi wa huduma za wanyama pori Julius kipng’etih amedhibitisha mauaji hayo ya simba 6 na kondoo 28, na kusema Simba hao walipotea kutokea hifadhi ya Nairobi.
“nilazima tuwakamate waliohusika na mauaji haya ya Simba, wanapaswa kupambana na sheria” alisema mkurugenzi huyo.
Simba hao waliua ng’ombe 8 siku ya jumatatu, na hivyo wakazi wa eneo hilo kukosa uvumilivu baada ya Simba kuua tena kondoo siku ya jumatano.

Post a Comment

Previous Post Next Post