ATLETICO YAENDELEZA UBABE, YAICHAPA 5 - 0 DHIDI YA WAW EL SALAAM

ATLETICO FC ya Burundi imeendeleza ubabe kwenye mechi za
Kundi C, za Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, baada ya
leo kuwafunga mabao 5-0 Waw El Salaam kutoka Sudan.
Waw Salaam waliofungwa na Yanga 7-1, sasa rasmi wameaga
mashindano hayo baada ya kupoteza mechi zote tatu, ya kwanza wakifungwa 7-0 na
APR ya Rwanda.
Kwa matokeo hayo, sasa Atletico inaendelea kuongoza Kundi C,
kwa pointi zake saba, baada ya kucheza mechi tatu, kushinda mbili na kutoa sare
moja, wakati APR ya Rwanda inashika nafasi ya pili kwa pointi zake nne na Yanga
ni ya tatu kwa pointi zake tatu, huku Waw Salaam ambayo haina pointi na imemaliza
mechi zake.
إرسال تعليق