Bao la ‘Boban’ kiboko -

BAO la kiufundi lililofungwa na Haruna Moshi ‘Boban’ dakika ya 66, katika mechi ya juzi dhidi ya Vita FC ya DR Congo, limemkuna kocha wake Milovan Cirkovic.
Milovan alisema juzi kuwa umahiri aliotumia kufunga bao hilo la kusawazisha kwa timu yake, limemfanya atamani kumpanga dakika zote 90.
Kauli hiyo imekuja huku Simba ikikabiliwa na mechi ya robo fainali dhidi ya Azam FC hapo kesho kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Milovan alikwenda mbali zaidi akilifananisha na mabao adimu yaliyofungwa kwenye michauno ya Euro 2012; katika fainali hizo, ambazo Hispania chini ya Kocha wake Vicente Del Bosque ilitwaa ubingwa kwa kuifunga Italia.
Milovan alisema licha ya Boban kutokuwa fiti, hivyo kusita kumwanzisha, anatamani kufanya hivyo katika mechi ya kesho.
“Boban ni mchezaji mzuri sana, ni mwenye umuhimu mkubwa katika timu, kinachofanya nisimwanzishe ni kutokana na kuwa fiti,” alisema Milovan.
Hata hivyo, Milovan alisisitiza wachezaji wake hawajaelewana kutokana na wachezaji wake wengi kutozoeana.
Alisema pamoja na changamoto hiyo, bado vijana wake watapambana kusaka ubingwa wa michuano hiyo huku akitoa wito kwa mashabiki kujitokeza kwa wingi kutoa sapoti.
Simba imeshinda mechi moja tu dhidi ya Ports ya Djibout na kufungwa mabao 2-0 na URA kisha kutoka sare ya bao 1-1

Post a Comment

أحدث أقدم