Nafikiria Ulaya - Okwi

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda anayekipiga katika timu ya Simba ya Tanzania, Emmanuel Okwi, amesema hana mpango wa kujiunga na timu nyingine nchini isipokuwa kucheza soka barani Ulaya.
Okwi amesema, hata kama mipango ya kucheza Ulaya itakwama, hatajiunga na timu nyingine nchini zaidi ya kuendelea kuitumikia Simba.
Akizungumza kwa simu kutoka nchini Uganda jana mchana, Okwi alisema anatarajia kuondoka nchini Uganda siku yoyote kwenda nchini Italia kwa majaribio kwenye klabu ya Parma iliyo Seria A.
Nyota huyo aliyezaliwa Desemba 25, 1992, alisema kabla hajafanikiwa Ulaya, yeye ni mali ya Simba, hivyo viongozi na mashabiki wasiwe na hofu.
“Ninashangazwa kuwepo taarifa kuwa nimejisajili na Yanga, mimi nipo hapa Uganda na leo hii (jana), natarajia kupata viza ya kuniwezesha kwenda Italia kwa majaribio,” alisema.
Awali, Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ alisema Okwi bado ni mchezaji wao, mkataba wake utafikia tamati mwaka 2013.
Kaburu amewasihi wanachama, wapenzi na mashabiki wa timu hiyo, kutokuwa na hofu juu ya mchezaji huyo anakwenda Italia kwa majaribio kwa baraka zao.
“Okwi ni kati ya nyota wenye uelewa mkubwa akitambua thamani na wajibu wake, hawezi kufanya mambo kama hayo yanayosambazwa kwa simu,” alisema Kaburu.
Kaburu alisema Okwi na beki wao Kelvin Yondan aliyejiunga Yanga, ni kati ya wachezaji wenye mikataba, hivyo kuhitaji mazungumzo kabla ya kuwachukua.
Alisema mbali na majaribio ya Italia ambayo kwa asilimia kubwa yatamuwezesha kujiunga nayo, Okwi pia amepata ofa nchini Ujerumani, Etoile Du Tunisia ya Tunisia, Mamelod Sundows na Orlando Pirates za Afrika Kusini.
Okwi ni kati ya wachezaji waliotoa mchango mkubwa kwa timu ya Simba kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara hadi kutwaa tuzo ya nyota bora wa kigeni

Post a Comment

Previous Post Next Post