BEKI
wa APR ya Rwanda, Buyi Twite na kiungo wa timu hiyo Jean Claude Iranzi
wamehusishwa na mpango wa kujiunga na klabu ya Yanga ya jijini Dar es
Salaam tayari kukipiga msimu ujao.Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kupitia mtandao mmoja nchini Rwanda, mikataba ya wachezaji hao wanaocheza APR ya Rwanda, inamalizika hivi karibuni.
Taarifa hiyo ilidai kuwa tayari Mbuyi na Iranzi wamefanya mazungumzo ya awali na Yanga ambayo imeonyesha nia ya kuwasajili.
Habari
zaidi zilidai kuwa Yanga ipo tayari kutoa kitita cha Franc za Rwanda
18milioni kwa ajili ya kumnasa Twite na Franc 7milioni ili kumtwaa
Iranzi.
Pia ilielezwa, mbali ya Iranzi kutakiwa na Yanga, klabu
nyingine ya Rayon Sports ya Rwanda nayo imekuwa imetajwa kuwania saini
ya nyota huyo.
Katibu Mkuu wa APR, Adolphe Kalisa amesisitiza
kuwa mpaka sasa hakuna mazungumzo yoyote yaliyofanyika kati yao na
wachezaji hao kuhusu kuongeza mkataba.
"Hatujafanya mazungumzo
yoyote ya kuongeza mikataba na wachezaji hawa mpaka sasa, tumeamua
kuacha kwanza mpango huu mpaka baada ya michuano ya Kombe la Amani
itakapomalizika," alisema Kalisa.
Akizungumzia mpango huo, Iranzi
alikiri kufuatwa na Yanga lakini akasema aliomba apewe muda ili aweze
kuelekeza akili yake kuisaidia APR kwenye michuano ya Kombe la Amani.
Mmoja wa waratibu wa usajili klabu ya Yanga, Seif Ahmed alipoulizwa kuhusiana na mpango huo, alisema hana lolote analofahamu.
Ahmed alisema taarifa hizo ni mpya kwake kwa vile hakuwahi kusikia mpango wowote wa kutaka kuwasajili wachezaji hao.
Mmoja wa waratibu wa usajili klabu ya Yanga, Seif Ahmed alipoulizwa kuhusiana na mpango huo, alisema hana lolote analofahamu.
Ahmed alisema taarifa hizo ni mpya kwake kwa vile hakuwahi kusikia mpango wowote wa kutaka kuwasajili wachezaji hao.
"Mimi
nachofahamu ni kwamba, kulikuwapo na mazungumzo kati yetu na
mshambuliaji wa Polisi ya Rwanda, Meddie Kagere," alisema Ahmed.
Kuhusu mazungumzo na Kagere, Ahmed alisema: "Mazungumzo yamefikia hatua nzuri, tunaelekea ukiongoni kumaliza mambo kabisa."
Kuhusu mazungumzo na Kagere, Ahmed alisema: "Mazungumzo yamefikia hatua nzuri, tunaelekea ukiongoni kumaliza mambo kabisa."
Wakati
huohuo, Kamati ya Uchaguzi ya Yanga imewataka wagombea watano wa
nafasi za uongozi wa klabu hiyo kuwasilisha vyeti vyao halisi vya elimu
kufikia saa 10 jioni leo ili vihakikiwe.
Wagombea hao ni Sara Ramadhani anayewania nafasii ya Uenyekiti, Abdalah Mbara, Edgar Fongo, Ahmed Gau na Shaaban Katwila wanaofukuzia nafasi za ujumbe.
Wagombea hao ni Sara Ramadhani anayewania nafasii ya Uenyekiti, Abdalah Mbara, Edgar Fongo, Ahmed Gau na Shaaban Katwila wanaofukuzia nafasi za ujumbe.
Akizungumza
jana, Mwenyekiti wa kamati, John Mkwawa alisema wagombea hao
wataondolewa kwenye orodha iwapo watashindwa kutimiza agizo hilo.
Mkwawa
alisema kuwa hatua ya kamati yake kuwataka wagombea hao kuwasilisha
vyeti hivyo inalenga kutekeleza agizo iliyopewa na Shirikisho la Soka
Tanzania(TFF).
Aidha, Mkwawa alisema kampeni kwa wagombea wa
uchaguzi huo zitaanza rasmi kesho na kuongeza kuwa wagombea wataruhusiwa
kunadi sera zao kuanzia asubuhi na hadi saa 12
Post a Comment