FERGUSON AMFAGILIA PATRICE EVRA, AKISAJILI MRITHI
MANCHESTER, England
KOCHA
wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amemsifu beki wake Patrice
Evra akimuita “askari kamili” – kauli aliyoitoa huku usajili wake wa
karibuni wa kinda Alexander Buttner ukitafsiriwa na wengi kama mrithi
wake Old Trafford.
Evra,
Mfaransa mahiri katika beki ya kushoto, amekuwa tegemeo la Mashetani
Wekundu kwa miaka sita ya uwepo wake klabuni hapo, lakini Fergie juzi
alimuonya beki wake mpya aliyemgharimu pauni milioni 4, Buttner,
kujipanga katika nafasi hiyo.
Bosi
huyo wa United alisema: “Tulichofanya ni kulinda matarajio yetu ya
baadaye. Hiyo ndiyo busara. Evra ana miaka 31 na Alex amekuja hapa kutoa
changamoto katika nafasi yake.
“Lakini
ikumbukwe pia kwamba hakuna mchezaji aliyecheza mechi nyingi kuliko
Evra katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Amefanya hivyo hata
katika mazingira magumu ikiwamo kuwa na majeraha.
“Amekuwa
mhimili wetu katika ulinzi akipanda na kushuka kwa miaka mitano. Ni
jumla ya mechi 240 alizocheza kipindi hicho, zinazomfanya sasa Patrice
kuwa askari kamili.”
Tangu uhamisho wake wa pauni milioni 5.5 akitokea Monaco
ya Ufaransa miaka sita iliyopita, Evra amecheza jumla ya mechi 291
akiwa na United, akitwaa kila taji na kujiwekea historia na heshima
kubwa katika soka la England.
Lakini
sasa Fergie yuko tayari kuanza kumbadilisha kwa kumtumia Buttner, 23,
Mholanzi aliyejiunga United akitokea Vitesse Arnhem, akifuata nyayo za
nyota wengine waliotua hapo kiangazi hiki, kina Shinji Kagawa, Nick
Powell, Angelo Henriquez na Robin van Persie.
Post a Comment