MADRID BINGWA SUPER CUP
![]() ![]()
Ronaldo
![]() |
Higuain |
MADRID,
Hispania
KLABU
ya Real Madrid imetwaa taji lake la kwanza la Super Cup ya Hispania ndani ya
miaka minne kufuatia mabao ya Gonzalo Higuain na Cristiano Ronaldo kuwapa
ushindi wa 2-1 dhidi ya Barcelona waliomaliza mechi wakiwa 10 usiku wa kuamkia
leo.
Ushindi
huo dhidi ya Barca, iliyompoteza Adriano aliyetolewa nje kwa kadi nyekundu
dakika ya 28 tu ya mchezo huo, ulifanya matokeo ya jumla ya mechi mbili za
kuwania taji hilo, yawe 4-4, baada ya Wakatalunya hao kushinda 3-2 katika mechi
ya kwanza Uwanja wa Nou Camp na Real wakapewa taji kwa sheria ya mabao ya ugenini.
Post a Comment