MADRID BINGWA SUPER CUP

MADRID BINGWA SUPER CUP

 Real wakiwa na Super Cup
Ronaldo
Higuain

MADRID, Hispania
KLABU ya Real Madrid imetwaa taji lake la kwanza la Super Cup ya Hispania ndani ya miaka minne kufuatia mabao ya Gonzalo Higuain na Cristiano Ronaldo kuwapa ushindi wa 2-1 dhidi ya Barcelona waliomaliza mechi wakiwa 10 usiku wa kuamkia leo.
Ushindi huo dhidi ya Barca, iliyompoteza Adriano aliyetolewa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 28 tu ya mchezo huo, ulifanya matokeo ya jumla ya mechi mbili za kuwania taji hilo, yawe 4-4, baada ya Wakatalunya hao kushinda 3-2 katika mechi ya kwanza Uwanja wa Nou Camp na Real wakapewa taji kwa sheria ya mabao ya ugenini.

Post a Comment

Previous Post Next Post