TETESI ZA UAMISHO/ MAGAZETI YA ULAYA

Scott SinclairManchester City watapambana kukamilisha usajili beki wa Inter Milan, Maicon mwenye umri wa miaka 31, kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.

Manchester City imeweka dau la pauni Milioni 6.2 kwa ajili ya winga wa Swansea, Scott Sinclair mwenye umri wa miaka 23.

Hamburg wamesema watafanya "lolote wawezalo" kukamilisha usajili wa kiungo wa Tottenham, Rafael van der Vaart, mwenye umri wa miaka 29, kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.

West Ham itajaribu kwa mara ya mwisho kumsajili mshambuliaji wa Liverpool, Andy Carroll, mwenye umri wa miaka 23, kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili na kuwapa fursa Wekundu hao kujaribu kumsajili mshambuliaji wa Arsenal, Theo Walcott.

Mshambuliaji wa Liverpool, Andy Carroll anajiandaa kuwa nje ya kikosi cha Wekundu hao kitakachocheza mechi ya Kombe la UEDA dhidi ya Hearts, habari zaidi zikisema ataondoka katika klabu hiyo.

Post a Comment

Previous Post Next Post