MAGAZETI ULAYA YA TETESI ZA USAJILI/UAMISHO -VITUKO ARSENAL

PAUNI MILIONI 30 ZA MAN CITY KUMTAKA DAVID LUIZ - CHELSEA WAZITOLEA NJE.

Jesus NavasChelsea imekataa ofa ya pauni Milioni 30 kutoka Manchester City kutaka kumnunua beki wao, wa Kibrazil, David Luiz mwenye umri wa miaka 30. City inakabiliwa na tatizo la beki, na Micah Richards anatakiwa kuwa nje kwa wiki 10 kwa sababu ya majeruhi.
 
 
Mmiliki wa Liverpool, John W Henry yuko tayari kuuzwa kwa viungo Charlie Adam na Jay Spearing -ili kutafuta fedha za kumnunua nyota wa Fulham, Mmarekani Clint Dempsey.
Habari kamili: Daily Mirror
 
Kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho amesema yuko tayari kumtoa kwa mkopo kiungo wa kimataifa wa Uturuki, Nuri Sahin katika klabu ya England, lakini hawezi kujali kama atakwenda Arsenal, Liverpool au Tottenham. 
Habari kamili: Guardian
Robert LewandowskiTheo Walcott akiwa amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake,  Arsenal inajipanga kwa lolote kwa kutaka kumsajili nyota wa Sevilla, Jesus Navas. Mchezaji wa kimataifa wa Hispania mwenye umri wa miaka 26 anaweza kuuzwa kwa pauni Milioni 35, lakini klabu yake inaweza kupokea fedha chini ya kiwango hicho.
Habari kamili: Daily Star
Klabu mbili za Milan, Inter na AC, zinagombea saini ya thamani ya pauni Milioni 8 ya mchezaji wa kimataifa wa Uholanzi,Nigel de Jong, mwenye umri wa miaka 27, kutoka Manchester City. De Jong, ambaye alijiunga na City akitokea Hamburg kwa pauni Milioni 18, Januari 2009, amebakiza mwaka mmoja tu katika mkataba wake Manchester na anaweza kuondoka.
Habari kamili: Goal.com
Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, Eduardo, mwenye umri wa miaka 29, amesema hakuwahi kujua kama alikuwa anatakiwa na Fulham kwa pauni Milioni 7, lakini amesema ni bora aondoke klabu yake ya sasa, Shakhtar Donetsk na kujiunga na klabu yoyote ya Ligi Kuu ya England.
Habari kamili: Independent  

Post a Comment

أحدث أقدم