NYOTA YA T. ULIMWENGU YAANZA KUNG'ARA MAZEMBE
Ulimwengu |
MAMBO
yameanza kumnyookea mshambuliaji chipukizi wa kimataifa wa Tanzania,
Thomas Emmanuel Ulimwengu baada ya kuingizwa rasmi kwenye kikosi cha
kwanza cha klabu yake, Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Kongo (DRC).
Ulimwengu
alikuwa kwenye benchi kwa dakika zote 90 jana wakati Mazembe,
ikiifunga Zamalek ya Misri mabao 2-1 kwenye Uwanja wa chuo cha Jeshi,
Al-Qahirah mjini Cairo, katika mchezo ambao, Mtanzania mwenzake, Mbwana
Ally Samatta ‘Sama Goal’ alifunga bao la ushindi dakika ya 44,
akiunganisha pasi ya Tressor Mputu Mabi.
Uli
alisajiliwa msimu uliopita Mazembe, lakini kwa muda wote amekuwa kwenye
kikosi cha wachezaji wa akiba hadi hapo jana, alipokaa kwenye benchi
kwa mara ya kwanza pamoja na kocha Msenegali, Lamine N’Diaye.
Katika
mchezo huo wa Kundi B, Himoonde alitangulia kuifungia Mazembe
inayofundishwa na Lamine N'Diaye dakika ya 34 pasi ya Mputu, lakini
Omotoyossi akaisawazishia Zamalek inayofundishwa na kocha Jorvan Vieira
dakika ya 36, pasi ya Mohamed Ibrahim.
Ushindi
huo wa kwanza ugenini kwa Mazembe katika hatua ya makundi, unaifanya
Mazembe ifikishe pointi saba, baada ya kucheza mechi nne, kushinda
mbili, sare moja na Berekum Chelsea na kufungwa moja na Al Ahly ugenini.
Al
Ahly iliyotoa sare ya 1-1 na Berekum Chelsea nchini Ghana leo, bado
inaongoza kundi hilo kwa pointi zake 10, wakati wababe wapya wa Ghana
wanashika nafasi ya tatu kwa pointi zao tano na Zamalek wanashika mkia
wakiwa hawana pointi hata moja.
Miezi miwili iliyopita, http://bongostaz.blogspot.com/ ilifanya
mahojiano na Makamu wa Rais wa Mazembe, Mohamed Kamwanya kuhusu
kuchelewa kwa Samatta kuingizwa kwenye kikosi cha kwanza, ambaye alisema
kwamba mshambuliaji huyo anachelewa kwa sababu kiwango chake bado
kidogo.
Alisema
kwamba, Ulimwengu kila anapopewa ruhusa ya kurejea Tanzania kujiunga na
timu za taifa, kwanza huchelewa kurudi Lubumbashi na pia hurudi akiwa
hayuko fiti.
“Hicho
ndio kinamchelewesha, lakini kama siyo hivyo angekuwa anacheza tu kama
mwenzake. Na nyinyi watu wa vyombo vya habari mtusaidie, kwa sababu
wachezaji wakija huko wanafanya anasa, wanarudi huku hawako fiti, sasa
inakuwa mbaya,”alisema Kamwanya.
إرسال تعليق