TBL YAZINDUA KINYWAJI KIPYA CHA "MALTIZA" KISICHO NA KILEVI



Meneja wa Kinywaji Kipya cha MALTIZA kinachozalishwa na TBL Bi. Consolata Adam akizungumza na vyombo vya habari kuhusiana na kuzinduliwa kwa kinywaji hicho kipya kinachopatikana katika ladha mbili za APPLE na PINE (Pineapple) ambacho amefafanua kwamba Tanzania imekuwa ya kwanza kwa Afrika kuzindua kinywaji cha aina hiyo kisicho na kilevi chenye ubora na kinachotengenezwa na kimea halisi kinachozalishwa hapa nchini.
Bi. Consolata Adam amesema kinywaji hicho kinapatikana katika ujazo wa 330Mls na kimeshasambazwa nchini kote na bei yake ni shilingi 1500, aliongeza kuwa kinywaji hicho ni halisi kisichotiwa rangi na kuwataka Watanzania kujiburudisha na MALTIZA.
Bi. Consolata Adam akionyesha kopo za Ujazo wa 330Mls za kinywaji cha MALTIZA aina ya APPLE na PINE

Post a Comment

أحدث أقدم